Mgombea urais kwa teketi ya CCM, Dk.John Magufuli amepata mapokezi makubwa mkoani Tanga katika wilaya zote alizotembelea ikiwemo Korogwe, Mkinga na Lushoto.
Akizungumza wakati wa kumnadi mgombea Ubunge wa Jimbo la Bumbuli Januari Makamba Dk. Magufuli amesema ikiwa atachaguliwa kuwa rais wa Tanzania ata hakikisha kuwa anaboresha maslahi ya watumishi wa majeshi ya ulinzi na usalama nchini kutokana na kutambua
mchango wao katika kulinda amani ya nchi yetu.
Ameongeza kuwa amepanga watumishi wa jeshi wawe na mishahara mizuri ili waweze kufanya kazi ya ulinzi na usalama wa nchi kwa ufanisi zaidi huku akitumia nafasi hiyo kuomba Watanzania kudumisha amani ya nchi.
Hivisasa joto la uchaguzi limepanda huku siku za kufanyika Uchaguzi mkuu zikiwa zinakaribia ambapo utafanyika tarehe 25 octoba mwaka 2015.
0 comments:
Post a Comment