CHOMBEZO UTAM WA BODA DODA SEHEM YA 1

JUA kali anti, panda twende,” dereva wa gari dogo aina ya Toyota Vitz alimwambia Mage huku akipunguza mwendo na kutembea naye sambamba.. . “Asante , nashukuru,” alijibu Mage huku mkono wake wa kulia akiwa ameutumia kuweka mkoba wake juu ya kichwa ili kuziba jua lililokuwa likimchoma alasiri hiyo.. . “Twende dada … ” “Nimesema asante jamani ah!” alisema Mage, safari hii kwa ukali kidogo . “Nisamehe anti kama nitakuwa nimekukera. ” “Tena sana tu, ” alisema Mage akiangalia pembeni . Dereva huyo aliongeza mafuta, akaondoka zake.. . “Mijitu mingine bwana , inaamini kuwa na gari ndiyo njia pekee ya kumpata mwanamke. Mwone kwanza, ” alisema mwenyewe Mage. Ni kweli 0 jua lilikuwa kali sana japokuwa ilipata saa tisa alasiri . Mage alikuwa akitembea kutoka nyumbani kwake Kimara kwenda kituoni kupanda daladala kwenda kwenye kikao cha harusi Kinondoni .. . “Da ! Lakini kweli jua ni kali sana, ” alisema moyoni, akatumbukiza mkono kwenye mkoba na kutoa kitambaa ili kujifuta jasho jembamba lililoanza kumchuruzika. Hatua kama kumi na tano tangu akatae lifti ya Vitz, Mage alipungia mkono Bajaj. .. “Unaweza kunipeleka Kinondoni ?” “Sawa .” “Itakuwa shilingi ngapi ?” “Elfu kumi tu. ” “Eti elfu kumi tu. Yaani elfu kumi we unaiona ndogo mpaka unasema tu? Mimi nina elfu nane tu. ” “Na wewe elfu nane unaiona kubwa mpaka unasema tu? Haya twende .” Mage alipanda akiwa anacheka majibu ya dereva huyo wa Bajaj .. . “Usikimbize please. ” “Usijali dada , mimi dereva mzuri sana .” “Ohoo! Wapo wenzako walisemaga hivyohivyo matokeo yake wakanitumbukiza kwenye mtaro ,” alisema Mage. “Kwani ni mara yako ya kwanza kupanda Bajaj anti?” “Ndiyo usafiri wangu mkubwa kila siku kama nina shida ya kwenda mahali .” “Basi kumbe utakuwa umejua Bajaj ni bora kuliko bodaboda . ..” “Tena usinitajie hao watu wa bodaboda . ” “Kwa nini anti ?” “Hawajitambui . Wanachojua wao ni kusukuma mbele bodaboda lakini si kujua wapi wapite, muda gani na mahali gani!” *** Bajaj iliendeshwa kwa uangalifu mkubwa mpaka Kinondoni , Mage akashuka alikotakiwa kushuka , akalipa akaingia kwenye baa ambayo ilikuwa na kikao. Aliwahi kwa vile yeye ni katibu. Wajumbe wa kikao walianza kuwasili mmojammoja, Mage akiwa ameshafika . Kila mjumbe alipofika yeye alimwandika jina na kumpa karatasi yenye maelezo ya kikao kilichotangulia. Miongoni mwa wajumbe waliokuwa wakifika , wengine walikuwa kwenye magari yao, wengine walishuka kwenye Bajaj , wengine na bodaboda. .. “Yaani hata wewe Martha unapanda bodaboda?! Huogopi ?” Mage alimuuliza Martha ambaye ni mjumbe wa kikao hicho. “Niogpe nini sasa Mage? Kuna usafiri mzuri na wa haraka kama bodaboda ?” “Mh ! Ajali je?” “Ajali ni bahati mbaya , mbona hata malori yanapata ajali, sembuse bodaboda!” “Da ! Mi sijawahi na sitaki kujaribu . Nitaendelea kupanda Bajaj mpaka basi.” Kikao cha harusi kilianza baada ya mwenyekiti wake kufika na wajumbe kukidhi akidi ! Kikao kilienda vizuri huku wajumbe, akiwemo Mage wakiruhusiwa kupiga ulabu watakavyo kutokana na fedha za uchakavu wa wiki iliyopita . Kidogokidogo wajumbe walianza kulewa , hata mazungumzo yao yaliashiria hivyo. .. “Sasa jamani nadhani tuje kwenye kipengele cha ahadi, kama kuna mtu anataka kutoa ahadi aseme , kama kuna mtu alishaahidi anataka kupunguza afanye hivyo, harusi yetu sote jamani ,” alisema mwenyekiti huku glasi yenye bia ikiwa mkononi tayari kwa kuipeleka kinywani.. . “Mimi wiki iliyopita nilisema nitatoa shilingi laki moja lakini leo naongeza na gari la kubebea wazazi wa bwana harusi ,” alisema mjumbe mmoja anaitwa Zakayo huku akinesanesa kwa ulevi. .. “Paa paa paa,” wajumbe walipiga makofi .. . Baadhi ya wajumbe walishangaa kwani wanavyomjua Zakayo hana hata baiskeli sasa kusema atatoa usafiri kwa wazazi wa bwana harusi kwao ilikuwa ni mshangao .. . “Labda atawakodishia,” alisema moyoni mwanamke mmoja aitwaye mama Maende ambaye ni jirani na Zakayo.. . “Mimi nitatoa usafiri kwa maharusi, kutokea kanisani hadi ukumbini na kutoka ukumbini kuwapeleka fungate ,” alisema mzee Majaribio huku sauti ikianza kutoka kwa kukawaruza kutokana na ulevi wa kuanza mapema . Huyu mzee Majaribio anamiliki magari mawili lakini mtaani anasifika kwa uchoyo wa lifti. Yeye hata kama kuna mvua, akimwona jirani anatembea kwa miguu anageuzia macho pembeni au kama atasimamishwa kwa kuitwa kwa sauti , atauliza. .. “Unaelekea wapi wewe ?” “Mimi kanishushe pale Rombo.. .” “Aaah ! Napita chuo , pole sana .” Hata kama hapiti chuo . Baadhi ya wajumbe wanaomfahamu walimshukuru Mungu kuona kama kweli mzee Majaribio ataweza kutoa gari lake kwa ajili ya maharusi . Na gari alilojua ni moja kwani ndiyo jipya . Saa mbili usiku, kikao kilimalizika, sasa ikawa maongezi ya wajumbe na bia juu . Mwenye kucheka alicheka, mwenye kulalia kiti sawa , Mage alikuwa akisinzia huku simu zake mbili zipo mezani. Saa tano usiku ilifika kama mchezo , wajumbe walianza kuchomoka mmojammoja bila kuaga . Mage naye alijikokota hadi kituo cha daladala kutafuta usafiri wa Bajaj .. . “Anti twende,” dereva wa bodaboda alimwambia
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: