Mgombea urais wa UKAWA Edward Lowassa ameonesha kusikitishwa na kitendo cha alio waita wapinzani kumuhujumu kwa kuchana mabango na kuyatupa porini katika maeneo mbali mbali nchini.
Akizungumza kwenye uzinduzi wa Kampeni za chama cha CUF Visiwani Zanzibar jana Lowassa aliyepewa dakika tatu kusema neno katika mkutano huo alisema wamebaini kuwa wapinzani wao wanachana mabango na kuyatupa porini.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti Mwenza UKAWA James Mbatia hivi karibuni alisema maeneo ambayo mabango hayo yaliondolewa na kuharibiwa ni Jiji la Dar es Salaam, Zanzibar na Iringa.
Licha ya kutoa kilio hicho Lowassa alitumia fursa hiyo kuwaomba wananchi hao, wawapigie kura yeye na Maalim Seif, huku akisisitiza `ushindi’ upo.
Katika kampeni hizo Dk. Maalim Seif amewaahidi wananchi visiwani humo kuwa endapo atashinda ataurejesha mchakato wa rasimu ya Katiba ya wananchi yenye maoni ya wananchi.
0 comments:
Post a Comment