CHOMBEZO RAHA ZABODA BODA sehemya 4

Mwili ulikuwa ukimsisimka kutokana na bodaboda kukimbia huku ikiwa kama inavaibreti kwa mbali ndiyo maana Mage alikuwa akihisi kusinzia na kujisikia raha kumwegemea dereva wake.Kwa vile ilikuwa ni usiku, Mage hakuona tatizo wala kikwazo mkono wake kuutumbukiza ndani ya suruali ya dereva huyo. Sasa akawa anashikashika na kuminyaminya kiasi kwamba dereva aliamua kupunguza mwendo na kuyumba barabara yote lakini hakutaka kusema lolote kwani upande wake alihisi starehe ya aina yake. Kwa vile alikuwa anapajua nyumbani kwa Mage, suka huyo aliwasha endiketa na kuanza kukata… “Nyoosha dereva, mpaka nitakapokwambia…” alisema Mage bila kutoa sababu ya kupitiliza kwa safari hiyo. “We twende tu,” alisema Mage mkono ukiwa umekomaa kule alikoshika na akiendelea kuminyaminya. Hapo suka aliegesha bodaboda pembeni akiwa hajiwezi… “Anti eee. Mimi siko vizuri, umenifanya mwili wangu uchoke, huoni kama unaniumiza?” “Jamani wewe, nakuumizaje sasa? Haya geuza bodaboda twende unipeleke nyumbani sasa,” alisema Mage.Suka.aliongeza mafuta hadi sehemu ya kona ya kukata kurudi alikotoka, akaongeza mafuta kuitafuta kona ya kwenda kwa Mage. Lakini Mage hakuacha tabia yake, bodaboda ilipokolea moto akapeleka tena mkono na kushika kulekule, safari hii kwa kupapasa kama vile anaogopa kuungua moto. Bodaboda iligoma kwenda, suka alizidiwa akawa anahangaika kwenye kiti chake. Kuna wakati alitaka kuiangusha bodaboda kwenye kichaka ili ambake Mage lakini kuna watu walikuwa wakitembea kwa miguu pemheni ya njia. Walipofika nje ya nyumba, Mage alisema… “Nashukuru sana kwa kunileta.” Hapo alikuwa akitoa pesa ya kumlipa… “Nitakuita tena kesho kuna harusi. Utanipeleka halafu baadaye utanirudisha, sawa?” “Saa ngapi?” “Saa mbili ndiyo nitakuwa nataka kutoka hapa nyumbani,” alisema Mage akiwa anapanda ngazi za kuingilia kwake huku nyuma wowowo lake likitingishika mithili ya mawimbi ya bahari. Suka alimwangalia weee mpaka akatingisha kichwa. Aligeuza bodaboda na kuondoka… “Hii kazi nayo ina majaribu sana. kuna yule mwanamke wa Ilala, yeye alikuwa akinibusu njia nzima. Halafu yule mwanamke wa Kigogo Mbuyuni, yeye alikuwa akiingiza vidole vya mkono wake kwenye mkanda wa suruali,” alisema suka huyo akiwa anaongeza mafuta kwa kasi baada ya kuingia barabara kubwa. Siku hiyo aliwahi kutoka kijiweni, akampitia demu wake aitwaye Madawa ili waende wote kwao baada ya kuamshwa joto la mahaba na Mage.Usiku Madawa alikutana na kashikashi za aina yake kutoka kwa dereva huyo. Kila mechi ilipoishia, ilirudiwa tena… “Mpenzi wangu una nini leo jamani?” “Hata mimi sijui, nilikumisi tu,” alisema suka huyo akipekecha pedeli za baiskeli ya kitandani. Mwanzoni Maua alihisi kero lakini ikafika mahali akaanza kuhisi vizuri na kukubaliana na mechi zilivyokuwa zikichezwa hasa upande wa mshambuliaji huyo.Ilifika mahali suka akawa ameridhika lakini Maua ndiye akataka ngoma iendelee kupigwa sambamba na kuchezwa kwa ufundi wa hali ya juu. *** Siku ilipita, ikaingia nyingine, mchana Mage alimwendea hewani dereva wake na kumkumbusha kuhusu mtoko wake wa usiku… “Nakumbuka…nakumbuka anti, nitakuja kama tulivyokubaliana jana,” alisema suka huyo, Mage akakata simu. *** Saa mbili juu ya alama usiku, bodaboda ilisimama nje kwa Mage, suka hakushuka bali alipiga honi mara tatu… “Nakuja,” Mage alijibu kwa sauti ya juu.Ndani ya dakika kumi, Mage alitoka akiwa amependeza kuliko siku yoyote aliyowahi kukutana na dereva huyo… Alivaa gauni refu lenye rangi ya maji ya bahari lililomkaa vizuri na kumchora umbo lale zuri la namba nane, chini aliingiza miguu yake kwenye viatu virefu vyeusi huku mikono yake ikishika kipochi na simu… “Samahani sana, nimekuchelewesha?” aliuliza Mage… “Hapana, mbona ni muda huuhuu tu,” alijibu suka huku macho yake yakitalii kwenye mwili wa mrembo huyo kuanzia chini kwenda juu… “Nashukuru sana kwa kunisamehe.” Mage alipanda, bodaboda ikaanza safari ya kumpeleka Mage kwenye harusi…. “Ni wapi anti?”“Pale Sabasaba, Temeke.” “Ok,pale sabasaba ya maonyesho sio?.” “Ndio,hapo hapo Dia” Bodoboda ilikaza mafuta vizuri, ikafika mahali Mage akaanza kuhisi zile hisia zakekwa vile ilikuwa usiku akaenda mbele zaidi kwa kujiegemeza kwenye mgongo wa dereva kama kawaida yake. Dereva naye alikuwa akiupenda ule mchezo.kwani mbali na kuwa kero hakuwa akimshutumu moja kwa moja msichana huyo. Mage alikiegemeza kifua chake kwenye mgongo wenyewe wa suka huku akiwa ameshaanza kujipinduapindua. Mara, akapeleka mkono mpaka kule mahali kwake. Alipoona hajashtukiwa akaupeleka ndani zaidi na kushika mbovumbovu.Dereva alivumilia sana lakini.safari hii aliweka lengo kwamba atakapomrudisha nyumbani ndiyo mambo yote yangejulikana… “Huyu leo ninaye, labda nisimrudishe mimi,maana sasa nitakuwa ni bwege sana,” alisema moyoni suka. “Mimi nakaribia kufika ukumbini?” alisema Mage huku akitafuta dakika tano tu za kumjeruhi kabla hajaenda ndani ya ukumbi. Safari hii alimkumbatia sana mpaka kufikia hatua ya Mage kumshika chuchu ambapo naye alilipuka kwa mshtuko…… ITAENDELEA…
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: