LHRC ‘yakemea’ kauli za Dkt. Magufuli


Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Dk.Helen Kijo-Bisimba.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Dk.Helen Kijo-Bisimba.
<a href='http://mpakasi.com/ads/www/delivery/ck.php?n=a3aba3f4&amp;cb=Math.random()' target='_blank'><img src='http://mpakasi.com/ads/www/delivery/avw.php?zoneid=18&amp;source=https%3A%2F%2Fmpakasi.com&amp;cb=Math.random()&amp;n=a3aba3f4' border='0' alt='' /></a> Hatimaye  kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kimekemea kauli zenye kuwajengea hofu wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kidemokrasia wa uchaguzi mkuu ujao.
Hatua  hiyo  inafuatia  Dk.John Pombe  Magufuli  kutoa mifano isiyoshabihiana na hali iliyopo nchini ikiwemo kufananisha Tanzania  na nchi zenye machafuko.
Kwa mujibu wa  taarifa yake iliyotolewa kwa vyombo vya habari imemtaka mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM, Mh. John Magufuli kufuta kauli zake ikiwemo ya kufananisha mchakato wa uchaguzi na vuguvugu la mabadiliko ya Libya pamoja na serikali yake kuwapiga risasi wahalifu wa kutumia silaha.

<a href='https://mpakasi.com/ads/www/delivery/ck.php?n=a09a5920&amp;cb=Math.random()' target='_blank'><img src='https://mpakasi.com/ads/www/delivery/avw.php?zoneid=19&amp;source=https%3A%2F%2Fmpakasi.com&amp;cb=Math.random()&amp;n=a09a5920' border='0' alt='' /></a>
Aidha kituo hicho kilichopo chini  Mkurugenzi Mtendaji Dk.Helen Kijo-Bisimba kimesema kauli hizo zinatoa vitisho kwa wapiga kura kinyume na demokrasia kwa kuwa huwezi kufananisha mabadiliko ya kimapinduzi ya Libya na umwagaji damu uliotokea huko na mabadiliko ya amani kwa kupitia mchakato wa uchaguzi za kidemokrasia.
Katika hatua nyingine taarifa hiyo imesema  kuwa kauli hizo za mgombea huyo ni za kukemewa kwa kuzingatia nchi na chaguzi zinaongozwa kikatiba na Katiba inakinzana kabisa na kauli zilizotolewa na kiongozi huyo.
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: