Habari zilizotufikia hivii punde ni kwamba aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Dk. Willibrod Slaa pamoja na familia yake wamekwea pipa kuelekea nchini Marekani na familia yake.
Taarifa hiyo imebainisha kuwa Dk. Slaa amekwishandoka nchini kuelekea Marekani pamoja na familia yake tangu jana jioni.
Inadaiwa kuwa akiwa nchini Marekani Dr Slaa atajiendeleza katika kozi fupi katika tasnia ya Sheria na Lugha.
Aidha,katika mahojiano yake na kituo cha televisheni cha Azam, Dk. Slaa amesema nyumba yake itakuwa chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi kutokana na vitisho ambavyo amekumbana navyo tangu alipoamua kuachia ngazi Chadema.
Dk. Slaa amesema licha ya kuwa nchini Marekani ataendelea kufuatilia yanayojiri nchini huku akiahidi kurudi kupiga kura tarehe 25 octoba 2015.
0 comments:
Post a Comment