Gwajima aibua mazito ya Dr. Slaa


Askofu wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima akizungumza na waandishi wa Habari leo katika Hoteli ya Land Mark jijini Dar es laaam.
Askofu wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima akizungumza na waandishi wa Habari leo katika Hoteli ya Land Mark jijini Dar es laaam.
Askofu wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amejitokeza na kujibu tuhuma zote zilizotolewa dhidi yake  ikiwemo kuitwa mshenga na Dk Wilbroad Slaa wakati akitangaza kujiuzulu  wiki iliyopita

Akizungumza na Waandishi wa Habari pamoja na wananachi wengine walio hudhuria katika mkutano huo Gwajima amesema kuwa kujiuzulu kwa Dr Slaa Chadema  sababu sio ujio wa Mwanasiasa Edward Lowassa aliyepewa ridhaa ya kugombea urais kupitia umoja huo.
Amesema chanzo ni mchumba  wake  Bi. Josephine Mushumbushi aliyepinga ujio wa Edward Lowassa  kwa kuwa aliona kwamba jina la Dr.Slaa litaenguliwa katika kinyang’anyiro cha Urais na kupewa Edward Lowassa suala litakalopelekea yeye kuukosa ‘ufirst lady’ kwa kuwa amesha waahidi ndugu zake na marafiki zake kuwa atakuwa mke wa Rais ikiwa UKAWA itapewa ridhaa ya kuchaguliwa kuiongoza Tanzania kwa miaka mitano ijayo.
Hatua hiyo imepelekea Bi Josephine kumzuia Dr.Slaa kuhudhuria mikutano ya Chadema wakati wa mchakato wa kumpokea Mwanasiasa Edward Lowassa hali iliyopelekea  pia Dr. Slaa kutupiwa mabegi yake nje na kulazimika kulala kwenye gari lake nje ya nyumba yake.
Akizungumzia kuhusu maaskofu kuhongwa na Mwanasiasa Edward Lowassa Gwajima amesema kwamba anachofanya Dr.Slaa ni kuwafanya maaskofu wasiheshimike mbele ya jamii kutokana na kuwahusisha katika kashifa wasiyohusiaka nayo.
Katika hatua nyingine Gwajima amesema anayo mambo mengine mazito ya Dr. Slaa ambayo akiyaweka wazi umma utashangaa hivyo kumtaka Dr. Slaa ajitokeze tena kumjibu ili yeye ajitokeze na kusema yote hadharani.

Ukumbi aliofanyia mkutano Mchungaji Josephat Gwajima leo.
Ukumbi aliofanyia mkutano Mchungaji Josephat Gwajima leo.
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: