FILIKUNJOMBE APITA BILA KUPINGWA JIMBO LA LUDEWA


Filikunjombe akiwasalimia wananchi wa mwambao wa ziwa Nyasa



wananchi wa jimbo la Ludewa wakimpokea Filikunjombe kwa shangwe na ndelemo

Mgombea ubungea wa jimbo la Ludewa katika mkoa wa Njombe kupitia tikeati ya chama cha mapinduzi(CCM) Bw.Deo Filikunjombe amepita bila kupingwa wilayani hapa baada ya mgombea  wa chama cha demokrasia na maendeleo(CHADEMA) kushindwa kutimiza  masharti na taratibu za ujazaji wa fomu za kuwania nafasi hiyo.

Msimamizi wa uchaguzi wilayani Ludewa Bw.Wiliam Waziri alisema kuwa mgombea wa Chadema alishindwa kutimiza taratibu za ujazaji wa fomu hizo hivyo kukosa sifa ya kuwa mgombea  wa ubunge hivyo kupelekea nafasi hiyo kujazwa na mtu mmoja ambeye alimtangaza rasmi Filikunjombe kuwa mbunge ambaye amepita bila kupingwa.

Bw.Waziri alisema kuwa katika kinyang’anyilo hicho wagombea waliochukua fomu walikuwa wakitokea vyama vinne ambavyo ni DP,TLP,CHADEMA na CCM hata hivyo wagombea waliorudisha fomu ni wakutoka vyama vya CCM na CHADEMA ambapo hata hivyo mgombea wa CHADEMA alishindwa kurejesha fomu ya kiapo cha maadili ya sheria za uchaguzi na kupelekea  kukosa sifa za kupitishwa kuwa mgombea.

Alisema kuwa mgombea huyo wa chadema ambaye alimtaja jina kuwa ni Bathromeo Mkinga alitakiwa kutoa maelezo ya kwanini aliondolewe katika kinyang’anyilo hilo lakini alishindwa kutoa maelezo yanayojitosheleza na kuishawishi tume  hivyo kupelekea Filikunjombe kupita bila kupingwa.

“Namtangaza Bw.Deo Filikunjombe kuwa mbunge aliyepita bila kupingwa katika jimbo la uchaguzi la Ludewa  kutokana na mgombea wa chadema kushindwa kukamilisha taratibu na masharti katika fomu na kushindwa kutoa maelezo kwa maandishi yaliyonyooka hivyo kama msimamizi wa uchaguzi namtangaza rasmi Bw.Filikunjombe kuwa mbunge wa jimbo la Ludewa”,alisema Bw.Waziri.

Bw.Waziri amewataka wananchi wa wilaya ya Ludewa kuwa watulivu na wenye busara katika kipindi hiki cha uchaguzi kwani kama wilaya ya Ludewa ilivyozoeleka kwani  kabla ya uchaguzi kulikuwa na maisha na baada ya uchaguzi kunamaisha hivyo hakuna haja ya kurumbana wakati wa kampeni za kuwasaka madiwani ili kulinda amani ya Taifa.

Hata hivyo wananchi wa wilaya ya Ludewa walisema kuwa hiyo ni laana inayowapata wapinzani kutoka kwa wazee wa Ludewa kwani awali wazee wa wilaya hii walionya kuwa hawahitaji mtu mwingine kugombea na atakayediriki kufanya hivyo wao watamshughurikia kikamilifu kutokana na Filikunjombe kuwafanyia makubwa wananchi wa jimbo lake.

Akieleza hayo mmoja wa wananchi hao Bw.Timoth Komba alisema kuwa kutokana na utendaji wa Filikunjombe wanaludewa hawakuwa na haja ya kuwa na watu wanaompinga mbunge wao hivyo yaliyowakuta Chadema wilayani hapa ni laana za wazee ambao walishatoa angalizo mapema kabla hata ya mchakato wa kura za maoni.

Aidha aliwataka wananchi wengine kuacha malumbano yasiyo ya msingi na kuendelea na shughuri zao za kujiingizia kipato kwani tayari mbunge amejulikana na mchakato wa kuwasaka madiwani ukiendelea hivyo kufanya uchaguzi usio na vurugu hasa katika kata ambazo zimewasimamisha wagombea wa udiwani wa vyama vya upinzani.

Mwisho.
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: