ZIARA YA KINANA NJOMBE

ninakuhabarisha kutoka ludewa njombe tanzania

NJOMBE
Katibu Mkuu wa Chma cha mapinduzi,CCM, Abdulrahman Kinana, amesema chama hicho kinawajibu wa kuisimamia serikali, katika kuhakikisha inapunguza urasimu na kuandaa mazingira mazuri, yatakayowawezesha vijana kujiajiri ili kuondokana na tatizo la ajira nchini.

Kinana aliyasema hayo, katika kijiji cha Isuka, wakati akizungumza na vijana 100, walioanzisha kituo cha mafunzo ya zana za kilimo, kwa wakulima wilayani Wanging'ombe mkoani Njombe, kwa lengo la kijishughulisha na kilimo cha mazao mbalimbali.



Alisema vijana wana nafasi kubwa ya kutumia fursa za kilimo ili kuendeleza maisha yao na baadaye kujiajiri badala ya kusubiria ajira na matokeo yake kujikuta wakiishi kwa matumaini bila ya kujua maisha yao yatakuwaje.

Alisema kuwa vijana wanatakiwa kukaa chini kufikiri na kuamua na kazi ya serikali itakuwa kutimiza mipango yao kwa kuwaandalia mazingira ya kujiajiri na kupata fursa za mikopo itakayowawezesha kuanzisha miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Dar es Salaam, leo kimeandaa mapokezi makubwa ya Katibu Mkuu wao, Abralrahaman Kinana , kufuatia kumaliza ziara katika mikoa ya Ruvuma, Mbeya na Njombe.
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: