CHOMBEZO; HEHEEE, KANTANGAZEEE!!! SEHEMU YA KUMI NA SABA



“Dobe nisikilize kwa makini sana. Huyo unaemwita Baby yule mtu mzima hovyo leo hii ninataka afilie mbali. Kwani yeye ndiyo kikwazo kwangu, na ninakuhakikishia ninamuondosha katika dunia hii, kwani najua atanitangaza tu!”
Meneja ananambia maneno hayo huku akiwa amechukia sana. Nikiwa nipo katika kuchanganyikiwa kwa maneno ya Meneja wangu, ninauona mlango unafunguliwa na mara anaingia mtu ambae hakika moyo wangu unapiga sarakasi ya Shufani kwa fadhaa!!!
“Dobe hujambo, mbona na Khanga kulikoni?”
Ninamsikia huyu mtu ananita kwa jina langu. Mie ndiyo mara yangu ya kwanza kumuona machoni mwangu, mashaallah mdada minal aal. Amependeza siyo kawaida yaani ni shidaa!
“Umenijuaje jina langu na umetambuaje kama nipo hapa?”
Mie nikiwa ninamshangaa huyu mrembo kwa uzuri wake hadi moyo wangu ukapiga sarakasi, ninashangaa zaidi ninapomuona Meneja wangu anamtazama mgeni huyu kwa mashaka! Meneja macho ameyatoa hana karibu wala habari. Mie nilidhani ni mshirika wake kumbe inavyoonekana ni watu wawili tafauti kabisa.
“Nani wewe na umefata nini hapa?”
Meneja anamuuliza huyu mgeni, huku akiwa ametaharuki vibaya sana. Kabla hajajibiwa chochote meneja wangu ananyoosha mkono wake kuichukua simu yake ili apige wapi sijui, lakini hafanikiwi. Mgeni anaupiga teke mkono wa meneja, simu inaanguka mbali na kutua chini ikiwa imesambaratika kila kitu sehemu yake.
“Angaifureni, mmachame unaejiingiza katika umafia usioufahamu madhara yake, unadiriki kukodisha genge la mabaunsa wakijifanya ni askari Polisi, unamtesa mtu na kumdhalilisha mbele ya jamii kwa tamaa zako za mwili tu, leo umefika mwisho wako shostito!”
Ninamshangaa huyu mwanamke simmalizi kabisa, lakini mie siku zote sijapata kulifahamu jina la meneja wangu hata siku moja zaidi ya kumwita bosi au Meneja, kumbe anaitwa Angaifureni, lakini hili la kuwa ni mchaga ninalifahamu sana, sasa huyu mdada ni nani hasa huyu?! Akili inanidulu.
“Nani kakutajia jina langu wewe, na umepajuaje mahala hapa?!”
Meneja Angaifureni anamuuliza huyu mgeni mrembo kwa wasiwasi mwingi. Huyu mgeni badala yakumjibu meneja wangu badala yake yeye anatabasamu tu. Anapofanya hivyo ninafanikiwa kuuona mwanya wake mzuri kinywani mwake. Ana rangi ya kahawia, ana midomo mipana, macho yake makubwa yanapendeza kulia kungu manga. Wanja mpana amepakaa katika nyusi zake, rangi ya mdomo ameikoleza inameremeta mdomoni. Hayo mavazi ndiyo usiseme ni balaa. Hakika pamoja na hapa nipo katika matatizo lakini, mwili wangu unasisimkwa kwa mwanamke huyu.
“Naitwa Qeenlyn George, tafadhali tosheka tu kwamba mie ni usalama wa raia na mali zao, wala hutakiwi kujua ninatokea kituo gani. Ila hapa nimemfata Dobe tu, sina shida na wewe Angaifureni, ingawa ukihitaji na wewe nikushughulikie basi nitafanya hivyo!”
Hili jina analojitambulisha nalo, Qeenlyn George, linaufanya moyo wangu unapiga pah. Ninamkumbuka Baby aliwahi kunambia kuja kwa mtu anaeitwa kwa jina hilo, akamjibu majibu ya kunya akainuka akapangusa makalio akenda zake, kumbe huyu ni askari?! Kwangu alisema ametumwa na Njasi huyu, ninamtazama kwa utulivu lakini pia kwa makini.
“Nisikilize bibie kwa makini, Dobe ni mfanyakazi wangu na bwana wangu pia. Hivyo ninaomba usituingilie katika mapenzi yetu”
Meneja anamwambia Qeenlyn maneno hayo kwa hamaki.
“Hehee, Kantangazee!!! Unanchekesha, Dobe hana akili akutake wewe? Mbele huchezi nyuma hutingishiki! Mja laana mjukuu wa mtwana, usiyejua maana! Sura kama mwanga wa mchana!!!”
Subuhana llah, huyu dada anamaneno mabaya namna hii, askari gani huyu? Yaani huyu ni shangingi hasa kama ni askari basi pia huyu ni mtoto wa mjini. Lakini pia shepu anayo mashaallah. Sasa ndiyo natambua kwa nini Baby Mwanamtama alimpa mineno ya shombo kumbe hakika anaweza kumwiba mtu huyu. Mie mwenyewe akitaka kuniiba aka wala sina neno, aniibe mchana kweupee Mbuzi anakula majani! Hata kelele za mwizi sipigi! Maana anaonekana ni mwingi wa habari.
“Samahani sana dada umekuja nyumbani kwangu ili kunitukana siyo! Basi ninakwambia tutaoneshana kama wewe askari mie ni raia ninaejiamini”
Meneja wangu anajitutumua kwa kusema kwa ukali.
“Dobe inuka nifate mie, tunakwenda wote hadi kituoni ili ukaandikishe maelezo yako ya kuvuliwa nguo na watu waliotumwa na Angaifureni, ukazalilishwa mbele ya umati wa watu, lakini pia kutekwa na kushambuliwa na watu hao.”
Ninapoambiwa maneno hayo ninainuka huku ninamtazama Bosi wangu mwenye jina kama dawa ya mchango wa uzazi!
Ninamuona nae ananitazama kwa chuki kubwa. Mie ninamfanyia ishara ya mikono kumuonesha kuwa sijui chochote.
“Dobe nenda hapo nje kuna gari nyeusi ina askari ndani yake, ingia humo mie ninamazungumzo kidogo na Angaifureni, kisha nitakuja ili twende sote kituoni.
Qeenlyn George ananambia maneno hayo mie nikiwa ninatembea taratibu kuelekea nje ya nyumba hii. Ninapotoka nje ninaiona gari nyeusi imeegeshwa na milango yake imefungwa, ina vioo vya kiza. Ninapoikaribia hii gari ninaona mlango wa nyuma unafunguliwa nami ninapanda ndani yake ninawakuta watu watatu. Nyuma wapo watu wawili, na dereva wa tatu. Kiti cha mbele cha abiria kikiwa kitupu nikafahamu kuwa hapo ni sehemu ya Qeenlyn. Hawa watu wamekaa kimya kabisa ninawasalimia lakini dereva peke yake ndiyo anaitikia salamu yangu.
Ninakaa kimya bila kuongeza neno, inapita kama dakika tatu hivi tangu mie nilipoingia humu garini, mara Qeenlyn anatokea na kuufungua mlango wa mbele kisha anamwambia dereva kwa kujiamini.
“Twende zetu.”
Gari inafunguliwa geti na mlinzi, inatolewa nje ya geti inashika njia ya Shekilango. Sote garini tumekaa kimya hakuna mtu anazungumza neno lolote. Mara simu ya Qeenlyn inaita nae anaipokea.
“Halow nambie wangu, eee, hapana hadi sasa bado ninamtafuta sijamtia machoni. Ndiyo hizo namba za gari ulizozitaja, tumeshazitangaza tunaitafuta hiyo gari. Akipatikana tu nitakujuza usijali wangu, vp na huyo Bibi anaendeleaje, weee dah huyo nae kujitia mpana kama pazia la Cinema, hee bibi anaupenda ujana na vijana huyo!”
Qeenlyn anamaliza kuzungumza na simu anaikata simu yake na kutulia kimya. Maneno hayo yananifanya nihisi kama vile walikuwa wakizungumza habari za Baby wangu, na kwamba ameshapelekwa hospitali. Ninajiuliza sana sipati majibu yake. Kwa nini Qeenlyn amwambie huyo aliekuwa akizungumza nae kuwa bado anamtafuta huyo mtu hajamtia mikononi?
Ninajiuliza kama sie mie ni nani? Inanijia kumbukumbu ya Njasi alipokuwa akizungumza na simu, wakati mie nishatiwa kwenye gari ya mabazazi. Lakini pia ninawaza kuwa huyu Qeenlyn na Njasi ni marafiki, ninajiuliza je kwani huyu ni askari wa ukweli? Isije ikawa tena jambo likahama kwa mjambaji likenda kwa mtema mate!
Dereva anakata kona ya kulia anaifata barabara ya Morogoro, anaingilia Ubungo maziwa. Tunachepuka kwani njia kuu imetawaliwa na foleni, tunatokea katika mitambo ya TBC ya idhaa ya nje, tunashika barabara ya Mandela tunaelekea Tabata. Gari inatembezwa kwa mwendo kasi watu tupo kimya kabisa hakuna mtu anaetia neno. Tunafika makutano ya barabara ya Tabata na Mandela, tunapinda kulia tunaelekea Tabata. Gari inaendeshwa kupitia njia ya Tabata ya Madson, tunakutana na barabara ya Tabata Mawezi, chombo kinakatwa kulia, gari inaendeshwa, hadi katika nyumba moja yenye geti jekundu, dereva anapiga honi, geti linafunguliwa chombo kinaingizwa ndani. Bado ninashangaa yaani ninatolewa sehemu moja ninapelekwa sehemu nyingine lakini kituo cha Polisi sipelekwi kabisa!
Nikiwa bado ninatafakari Ninatakiwa kushuka ndani ya gari, ninashuka ninatembea kwa taratibu na Khanga yangu kiunoni kama shoga.
Ninaingizwa ndani ya nyumba kisha gari inaondolewa ndani ya geti inashika njia. Qeenlyn ananifungulia mlango ninaingia katika chumba kimoja chenye choo ndani, ananambia
“Kwanza ingia huko ukajimwagie maji, upige mswaki kisha unywe chai, ndiyo tuzungumze yangu”.
Hakika nilikuwa ninayahitaji sana maji ya kuoga, kwa wakati huu, kwani mwili wote ninausikia unanata kwa jasho. Kinywa kizito kwa vile bado sijapiga mswaki asubuhi. Ninaingia bafuni ninajimwagia maji, ninaikuta miswaki mipya mitano imewekwa katika kidude maalum kilichokuwa na sabuni, dawa ya meno, pamoja na shampoo. Ninauchukua mswaki mmoja wa winsdom ninauweka dawa ninapiga taratibu. Ninapomaliza kujisafisha ninatoka chooni, ninagusa chumbani ninakuta chupa ya chai imewekwa kitandani, pia katika sahani ya udongo kumewekwa mikate. Nikiwa najiuliza hii chai ndiyo yangu mie, mara anaingia chumbani Qeenlyn akiwa amevaa mtandio wa dera akiufanya kama Khanga. Ameufunga mtandio kati ya kifua na mapaja, lakini namna mtandio ulivyokuwa mwepesi, ulikuwa unaruhusu chupi nyeupe aliyovaa, kuonekana kwa wazi kabisa ndani. Shanga chekwa zimebarizi katika kiuno chake. Nikiwa ninamtazama kwa mshangao anainua kinywa chake ananambia.
“Dobe usishangae wangu, shoga yangu Njasi keshakutangaza kwangu tayari, amenambia kila kitu kuhusu mautamu yako, na mie nipe utamu huo ndiyo shida yangu kwako! Yeye Njasi ndiyo alienambia kama wewe umekamatwa na Polisi, ila namna alivyonambia maumbile ya hao Polisi, nikampigia Best wangu mmoja yeye baunsa wa Las Vegas Casino huwa anatumiwa sana na watu kujidai kuwa ni askari, akanambia kuwa amehusika katika oparesheni ya kukukamata, na yeye ndiyo aliekukamata kiuno kukuelekeza nje kwenye gari. Siyo polisi wale. Wale ni wajanja tu na yeye ndiyo alienambia kama upo pale amenieleza hadi pesa waliyopewa, na gea yakuingilia pale, ndiyo maana na mimi pia nikaja na gea za uaskari, lakini mie hata CCP sijakanyaga wala huo uaskari haunihusu! Ila nimefanya hivi kwa kuwa shoga yangu Njasi ameumia sana, kwa hiyo malipo yangu kwako Dobe ni hicho kichwa cha samaki tu upo?!”
Anaposema maneno hayo anainua chupa ya chai ananitilia chai katika kikombe, kisha ananigeukia na kuniuliza.
“Bwana Dobe, unatumia sukari vijiko vingapi?”
Ninamtazama huku ninatabasamu ninamjibu.
“Vijiko vidogo vitatu, mie ninapenda sana sukari kama Mmanyema vile.”
Qeenlyn anatabasamu vijishimo vidogo vinatokeza katika mashavu yake. Mdomo wake mzuri, ninauingiza katika fikira zangu vipi kama mdomo huu ukiwa unanyonya Mkuyati? Nikiwa katika fikira hizo, ninauhisi mkuyati wangu ukichachamaa!
Qeenlyn ananiwekea sukari anakoroga kisha ananikaribisha.
“Karibu Shada mgombewa!”
Ninatabasamu huku nikitikisa kichwa kwa masikitiko kuitwa jina hilo. Ninakunywa chai kwa pupa kwani njaa ilikuwa inanisumbua sana, sema kwa matatizo niliyokuwa nayo sikuwa ninaifikiria namna ya kuitibu bali nilikuwa nayafikiria matatizo yangu.
Ninamaliza kunywa chai, ninaomba maji naletewa maji ya Baridi lita nzima, ninayakata yote. Naona jasho jembamba linanitoka.
“Samahani Qeenlyn, naomba unijuze hali ya Mwanamtama inavyoendelea kwani mie ndiyo sababu, nilipowaambia kuhusu Nge yeye na Njasi wakaanguka ndipo mshituko ulipompata.”
Qeenlyn ananitazama kidogo kisha ananambia.
“Baby wako anaendelea vyema kwani yupo hospitali amewekewa drip na hali yake inatengemaa. Haya unahitaji kujua nini tena Dobe?”
Mie ninafarijika sana anaponambia hayo.
“Sina jipya Qeenlyn nimemaliza labda kama wewe unalo la kunambia nakusikiliza.”
Qeenlyn anaondosha vitu nilivyotumia kwa chai, kisha anapanda kitandani, anajilaza ananitazama kwa macho ya huba. Hakika moyo wangu kwa huyu Qeenlyn, unakamatwa mzima hautoki. Nami ninapanda kitandani namsogelea karibu yake, tunatazamana usoni.
“Dobe usinibanie tafadhali, na mie nataka utamu, nipe kwa kadiri ya maujuzi yako.”
Qeenlyn ananiambia maneno hayo kisha ananibusu busu zito la uso. Akili yangu inacheza kidogo kwa busu lake. Ninaipeleka mikono yangu katika mwili wake, ninampapasa nje ya mtandio kisha ninaufungua juu ya kifua chake ninayaona matiti yake mazuri kwa kunyonywa yanaonekana bila khiyana, Ninapeleka ulimi wangu kifuani kwake, ninamnyonya chuchu moja na ya pili ninaichezea kwa mkono wangu, mkono wa pili nimeuzungusha unaumalizia kuushusha mtandio.
Qeenlyn ana joto jingi mwilini mwake. Ninaendelea kuushusha mkono wangu hadi kwenye chupi yake, ninaivuta na kuiachia inampiga mpira wa chupi kiunoni mwake.

ITAENDELEA








Ludewa yetu na maendeleo yetu posted by barnabas njenjema, kutoka Ludewa
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: