CHOMBEZO; HEHEEE, KANTANGAZEEE!!! SEHEMU YA KUMI NA NANE



+255718603654

Ninapeleka ulimi wangu kifuani kwake, ninamnyonya chuchu moja na ya pili ninaichezea kwa mkono wangu, mkono wa pili nimeuzungusha unaumalizia kuushusha mtandio.
Qeenlyn ana joto jingi mwilini mwake. Ninaendelea kuushusha mkono wangu hadi kwenye chupi yake, ninaivuta na kuiachia inampiga mpira wa chupi kiunoni mwake.
Ninamuingiza mkono ndani ya chupi ninatalii kwenye makalio, ninamuona hasisimkwi sana. Ninalitambua hilo ninauhamishia mkono wangu mbeleni kwake. Ninamshika Ukeni anaruka na kutoa mguno.
“Aaaagh”
Ninatambua huyu nyege zake zimebarizi huku chini. Ninamchezea kinembe kwa muda, huku ninamnyonya chuchu moja, na ya pili nikiichezea kwa mkono wangu wa pili.
Qeenlyn anasisimkwa sana, yaani anahangaika macho yake makubwa yanalegea yanazidi kuupamba uso wake. Ninaliachia titi lake kulinyonya, ninashuka bondeni ninaivua chupi yake kwa meno. Huku mikono yangu inapapasa chuchu zake kwa ufundi, na eneo lote la kifua.
“Hakika nimekubali Dobe wewe ni fundi, asante sana nipe raha hizo na mie.”
Qeenlyn ananambia maneno hayo, nami ninajisemea kimoyo moyo kuwa hapa ndiyo kwanza mkoko unaalika mauwa!
Mara tunasikia mlango umefunguliwa hamadi, tahayari inatujaa usoni!!!
Moyo wangu unaniripuka, kwani mtu anaeingia humu ndani ndiyo nyongo mkalia ini wangu. Ninamuona tofauti na fikira zangu, kwani anaponiona wala hashituki, isipokuwa anatikisa kichwa chake huku machozi yakimtoka mfululizo.
“Nisamehe shoga yangu, kwani na mie nilikuwa nautaka utamu wa Dobe, hivyo usilie siyo kama nimekusaliti, ila shetani na nyege zimenishinda nguvu shoga yangu.”
Qeenlyn anamwambia Njasi alieingia chumbani macho yake yakiwa mekundu sana.
Ninaacha kabisa kuendelea kucheza pambano, kwani Njasi ameharibu hali ya hewa, lakini pia analia tu. Ama kweli fumanizi baya hasa kwa mtu umpendae, kwani unaweza kufanya maamuzi mabaya kabisa.
“Njasi hatujafanya kitu lakini, ndiyo tuli………!”
“Kelele Dobe! Mmefanya hamjafanya mie hainihusu kimpango wenu!”
Njasi anasema kwa ukali huku machozi yanaendelea kummwagika machoni mwake.
Ninainuka nikiwa uchi, ninamfata aliposimama akituangalia huku analia, lengo langu nimtake radhi kwa sababu ya kumtia uchungu. Ninapomfikia ninanyoosha mkono wangu ili nimshike mkono nimkumbatie kisha nimpe Matentelee ashuke, lakini ninachezea bonge la kibao cha shavu!
Ninakamata shavu langu, alama ya vidole ninaiona imetokelezea. Ninatambua Njasi amechukia sana, lakini angempiga shoga yake siyo mie, kwani mie nilikuwa nimekamatwa na wale washenzi, sasa nimempataje, au katika mazingira kama haya yaliyonitokea ningewezaje kukataa?
“Njasi ni hili tu au kuna lingine?!”
Ninamuuliza kwa upole kwani kibao chake kimeniingia sana, na sasa ninalihisi shavu langu linanichonyota kwa maumivu.
“Njasi shoga yangu nisamehe mie, na ikiwa unataka kunipiga naomba unipige mie. Hakika Dobe utamuonea bure kwani mie nimemtoza nguvu hadi kunifanyia haya, na sikua na namna ila kutaka kupata utamu wake ule uliousema. Unajua tena sie wanawake tukiambiwa fulani mtamu kama nini, basi kama mie utamu nyumbani kwangu haupo, ninataka sana na mie nipewe huo utamu, hivyo yaliyopita si ndwele, tugange yaliyopo na yajayo.”
Qeenlyn anamwambia Njasi huku anavaa chupi yake na mtandio wake vizuri, kisha anamfata shoga yake anamshika mkono anamketisha kitandani. Njasi hawi mbishi kwa shoga yake, ila kwa kushikwa na shoga yake sasa analia kilio cha kwikwi.
“Qeenlyn apa haki ya Mungu kama kweli hujafanyana na Dobe.”
Njasi anasema maneno hayo huku uso wake umerowa machozi.
“Haki ya Mungu tena sijafanyana nae, alikuwa ananiandaa tu hata hatujatembea shoga yangu. Huo utamu wenyewe basi siutaki tena ushanitumbukia nyongo.”
Qeenlyn anamwambia shoga yake huku akimfuta machozi.
“Kama hujatembea nae kweli, basi mshukuru sana mungu wako.”
Njasi anaposema maneno hayo, ninamtazama kwani sijamuelewa kabisa anamaanisha nini hasa.
“Kwa nini unasema hivyo shoga yangu?!”
Qeenlyn anamuuliza Njasi nami ninakaa vyema kumsikiliza maana naona anataka kumuondoa shoga yake katika upendo wangu.
Njasi badala ya kusema analia sana kwa kwikwi kisha anashika mashavu yake kwa kukata tamaa.
Mie ninaona ni wivu wake tu, ndiyo maana analia kwa uchungu, na anakuwa katika hali hii.
“Shoga yangu, Dobe tumuogope kuliko Ukoma!”
Njasi anasema maneno hayo ananitia fadhaa sana.
“Njasi kwa nini unasema maneno hayo, au unanitilia zege mie? Lakini mie nishakuachia mpenzi wako na kama nilivyokwambia mie sijafanya nae mapenzi hasa zaidi yakuniandaa tu nakubahatika kuishika mashine yangu tu, lakini dudu hajanipa shoga.”
Qeenlyn anamwambia Njasi maneno hayo huku akiwa hamuelewi kabisa.
“Mwambie kweli shoga yako, kwa nini mniogope kama Ukoma?! Njasi wewe uliekuwa unalia wakati mie nimekamatwa! Ni wewe uliehakikisha hadi umefanya mapenzi na mie, leo nimekuwa niogopewe kama Ukoma?!”
Ninasema maneno hayo huku ninatabasamu siyo kwa furaha, ila kwa kuuona uongo dhahiri unaotaka kutengezwa nae. Kwani nimeona utangulizi tu ameaanza hivi haya akiingia katika sura ya kwanza, si ndiyo ataniuwa kabisa?
“Qeenlyn wewe ni rafiki yangu sana hadi tumekuwa ndugu na siyo marafiki tena. Natambua kwamba urafiki huisha lakini udugu kamwe hawishi. Kwani wazaramu wamepata kulonga kuwa, udugu jambo bora, kula chako nile changu, siku ya mashauri tuwe pamoja udugu jambo bora! Hivyo ninakwambia kuwa Dobe siyo mzima kabisa.”
Njasi anaposema maneno hayo, ninamtazama sana kwa jicho kali kisha ninasema kwa kujiamini.
“Njasi tafuta njia nyingine ya kumfanya shoga yako asiwe na mie lakini huko kuzuliana maradhi, tafadhali sana sipendi ujue.”
Njasi kwa mara ya kwanza anatabasamu usoni mwake tangu aingie humu ndani, kisha ananitazama kwa kunisikitikia. Ananambia kwa utuo maneno yake yaniingie.
“Dobe hakika nilikupenda sana, lakini kufikia sasa sina upendo hata kidogo na wewe. Tambua ushaumizwa na Baby wako. Mie ninatoka hospitali punde kumpeleka, kwa bahati nzuri pale hospitali kuna dakitari ninafahamiana nae, aliponiona akaniuliza nina matatizo gani, nikamwambia kwamba nina mgonjwa nimemleta amepata mshituko, dakitari akanitaka nimuoneshe mgonjwa wangu, hivyo nikenda nae hadi kwa mgonjwa mwenyewe nikamuonesha. Nilipomfikisha kwa Mwanamtama, kumbe dakitari anamfahamu matandu na makoko. Basi kwa kuwa mgonjwa alikuwa ametundukiwa dripu, tukatoka nje akaniuliza nipoje nae yule mgonjwa, nikamwambia nimetoa msaada tu wakumpeleka hospitali sipo nae vyovyote, ndipo aliponichana habari zote za Mwanamtama, hapa nilipo uchi wangu nimeuchukia kupita maelezo!”
Njasi anapofika hapo ninakohoa kisha ninafikiri kwa haraka ninaona hawezi kutunga uongo huu, kwani hakutarajia kama mimi atanikuta na Qeenlyn hivyo inawezekana maneno yake yakawa na ukweli ndani yake.
“Ehee shost, habari zake zipi hizo, maana ushanitia wahaka hapa na shengesha juu!”
Qeenlyn anamuuliza Njasi nami ninatoa macho tu kama Ng’ombe aliekuwa mnadani.
“Amenambia Baby Mwanamtama, mumewe amekufa na maradhi ya Ukimwi. Na baby alipopima pia amegundulika na Ukimwi miaka mitatu nyuma, na sasa anatumia dawa za ARV, anaishi kwa matumaini. Amenambia kuwa mtu mwenye virusi akipata mshituko kidogo tu, kinga zinashuka sana kwani anakuwa hafikirii kitu ila anawaza Ukimwi tu. Haya na mie huo mchezo niliocheza kwa pamoja na yule mama nitasalimika kweli!”
Njasi sasa ameuwa band kabisa. Mapigo ya moyo yananienda mbio kama saa mbovu. Mate yananikauka kinywani mwangu, sauti haitoki, kikohozi pia kinagoma.
“Njasi umesema mumewe Mwanamtama kafa na ugonjwa gani?!!!”
Ninafanikiwa kuyapata maneno, ninamuuliza swali hilo kama vile sijamsikia alivyosema awali. Nimetaharuki siyo mchezo, Ukimwi tena! Ninapandisha mikono yangu juu ninashika kichwa changu. Ama kweli kila mwenye kulia, anashika kichwa chake!
“Shoga kwani huyo mama umeshere nae Dobe, wewe si ulinambia alikuandaa tu kule kwenye massage hajakufanya?!!”
Qeenlyn anamuuliza shoga yake ambae sasa anatoa machozi mwa mwa mwa machoni mwake.
“Pale mwanzo hakika nilikuwa sijatembea na Dobe, ila ile Plan B, ndiyo nilipoitumia leo hii, yaani ndiyo mara yangu ya kwanza napewa mkuyati na Dobe, na leo hii hii nahisi nimeuvagaa tayari. Yaani ninajuta kwa nini sikutumia kinga. Siku hizi kuna condoms za kike kama mwanaume hapendi au hataki kuvaa mpira, mwanamke unavaa, lakini wapi nimefanya ngono zembe sasa inanigharimu, ama kweli sikio la kufa halisikii dawa! Ninajuta majuto ya firauni. Burudani ya mara moja inaniingiza katika matatizo ya milele aaaagh!”
Njasi anatungua kilio kikubwa sana. Mie nimejiinamia sina raha moyoni mwangu, sina amani, sina neno. Niyapate wapi maneno wakati Njasi keshasema hadi Tamati.
“Daaah shoga yangu pole sana, kama ndiyo hivyo miwaya ushaikanyaga hiyo mwaya! Ila ninakushauri nenda ukapime asaa kheri unaweza ukawa hujaumia, kwani ulipokuwa unapewa Matentelee ulichubuka?!”
Qeenlyn anamuuliza shoga yake mie sina wakuniuliza, nipo peke yangu kama Ng’ombe aso pembe!
“Shoga wee, nimejitia ufundi wa kunyonya dudu pamoja na yule kizee, kumbe ana manyenyele sasa ananichagiza kwa mawazo. Haya dudu nimechangia leo, hata nikipima nitaonekana ninao kweli? Si hadi ipite miezi takribani mitatu? Mie miezi miwili nyuma nilikwenda kumtolea damu mgonjwa, nikapimwa damu yangu ikakutwa salama. Damu yangu ni group ‘O’ hivyo ilimfaa sana mgonjwa ambae nae alikuwa na damu kama group yangu, hivi ingekuwa damu yangu inawadudu angewekewa yule mgonjwa kweli, hao madakitari wamekuwa wana vichaa basi!”
Njasi anazidi kujithibitisha kuwa yeye ni mzima wa afya kabla yakukutana na mie leo asubuhi.
“Dobe out!”
Qeenlyn ananambia huku hanitazami usoni.
“Unasema?!”
Ninamuuliza kwani keshanichanganya huku Tabata Mawezi na mie ninakaa Tabata Segerea haya ninaendaje na huu upande wa Khanga asubuhi hii?
“Ninasema toka nje ya nyumba yangu.”
Qeenlyn anayarudia maneno yake kwa msisitizo.
“Samahani naom……..!”
“Out!!!”
Simalizii kauli yangu Qeenlyn ananikatisha. Ninamtazama kwa macho ya kutia huruma, lakini huruma inavuka bahari inakuwa mbali sana kwake. Anainuka anaifata Khanga yangu ananirushia kisha ananifungulia mlango ili nitoke nje.
Ninavaa Khanga yangu kiunoni kisha ninamtazama Njasi ili kama vipi japo anipe pesa ya taxi ili nipande Taxi nisiadhirike lakini anatizama pembeni keshavurugwa.
“Naombeni nauli basi nitaendaje katika hali hii jamani”
Ninaposema hivyo Njasi ndiyo analala kabisa kitandani. Kama niliemwambia apumzike. Ninashika njia taratibu ninatoka chumbani humu nilipoingia bila hodi, hatimae sasa ninatoka bila kwa heri.
Ninapotoka nje ya chumba Qeenlyn anaufunga mlango wa chumba chake, kisha ananifungulia mlango mkubwa wakutokea nje ya nyumba.
“Qeenlyn nitazame hali yangu lakini, sina nguo, sina pesa, nitaendaje Segerea, basi bora ungeniacha kwa bosi alietaka kunipa maisha. Kuliko mhadhara huu mnaonipa.”
Ninamwambia kwa huzuni na huruma lakini nilikuwa natwanga maji kwenye kinu. Au niseme ilikuwa kama nasomea maiti niondoke na Ujaka wangu. Sikupewa majibu wala pesa, bali nilikuwa ninafanyiwa ishara yakutoka nje ya nyumba. Dah Dobe mie niliekuwa ninagombaniwa, leo ninasusuikwa kama Paka aliekunya?!
Ninatoka nje ya nyumba ninaingia mtaani taratibu machozi yananilengalenga huku watu wakinitazama kwa wasiwasi. Wapo walioniona nina upungufu wa akili, lakini pia wapo walioniona labda nimefumaniwa, ndiyo nimetolewa nduki. Lakini kuna dhana ya tatu hii siipendi kabisa nidhaniwe hivyo. Eti wapo walionidhania mie kuwa ni shoga! Kisa tu huu upande wa Khanga niliovaa! Aaah mie siyo shoga jama ni majanga tu yamenipata, mie ninaliza watu kwa furaha ila leo ninalizwa mie. Ama kweli kutesa kwa zamu. Ninatembea huku ninajiuliza itakuwa vipi kama kweli nikiwa nimeathirika? Nitakuwa mgeni wa nani mie, kwani kazini nishaharibu, kwa Baby nae ndiyo ameshayakanyaga mawaya sasa ninafanyaje?
Mara gari inanikosa kunigonga inakanyaga breki zinasota, ninakimbia pembeni kwa fadhaa na taharuki kubwa, upepo wa gari unaikudua Khanga niliyovaa ninainama nikiishikilia kwa nguvu isitoke kabisa nikawa uchi kabisa.
Nilipokuwa ninawaza huku ninatembea kumbe nilikuwa nipo karibu na barabara kubwa ya lami na ikawa ninaingia kati ya barabara sina habari. Ama kweli kuchanganyikiwa kubaya. Dereva wa ile gari anashuka katika gari yake ananifata nilipo ananiwasha vibao na matusi juu.
Mie simlipi tusi wala kurejesha pigo, kwani kweli kosa ni langu, hivyo mie ninamuomba radhi tu. Hatimae ananitazama huku akiwa amefura kwa hasira.
“Wewe unamatatizo gani wewe eee? Huo unga mnaokula na mibange yenu angalieni bwana mtakuja kufa mtupe matatizo tu!”
Ananambia maneno hayo kisha huyoo anakwenda kwenye gari yake anaingia kisha kabla hajaiendesha anashuka nakunifata tena. Ninahisi sasa ndiyo mitama inakuja kuchukua nafasi yake.
“Broo kwani wewe unakaa wapi?!”
Ananiuliza aliponifikia, huku mie nikiwa nimeshaitanua miguu yangu kujiandaa kwa mitama.
“Ninakaa Tabata Segerea.”
Ninamjibu bila kumtazama. Mara inasimama gari karibu kabisa miguuni mwangu, kisha inashusha kioo kilichokuwa kimefungwa ninamuona dereva akiwa ameshikilia usukani. Ananiashiria kupanda ndani yake.
Kwa kuogopa aibu ya barabarani, kujaza watu, hatimae kupigwa picha na kuwekwa kwenye mitandao ya kijamii, ninaamua kufungua mlango wa mbele wa gari iliyosimama ninaingia ndani yake, bila kuuliza mara mbili.
Gari inaondolewa eneo hilo huku kundi dogo la watu waliokuwa wamenijalia ninawaona wananicheka bila kufahamu mwenzao nimetingwa na jambo gani.
Ninamtazama dereva wa gari ninavuta kumbukumbu usoni mwake, lakini sikumbuki kabisa kama nimemuona wapi mtu huyu. Yeye amenyamaza kimya anatia gia tu hana habari na mie. Ninataka kumsemesha mara moyo wangu unapatwa na mstuko, nyuma ya kiti nilichokaa ninasikia sauti ikinisemesha.
“Dobe hatimae leo tumekutana tena!”

ITAENDELEA KESHO KATIKA MUDA WAKE.




Ludewa yetu na maendeleo yetu posted by barnabas njenjema, kutoka Ludewa
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: