SECONDARY SCHOOL sehemu ya 10


SECONDARY SCHOOL

Sehemu Ya 10

Mtunzi..... MoonBoy

Simu No. +255714419487 WhatsApp

Ilipoishia Jana →↓↓

kinyume nyume eti niduu nae na wakati ni wakiume....
"skieni washkaji"
"nini dogo kama ni pesa tutakupa kikubwa utufikishe mzigoni"
"sikieni basiiiii"
"tusikie nini wewe mkamue mwana uyooo"
"Oyaaa mimi ni mwenzenu nipo kama nyie rafki zangu"
"Eti nini??? yani na wewe pia upo kama sisi? sasa kwanini tusijiunge pamoja upige pesa dogo?"

SONGA NAYOOOOOOO



Nilijikuta nikiwa na kigugumizi cha hapa na pale kuhusiana na hilo la kwenda kupiga kazi kutokana hali niliokua nayo,
"amna unajua mimi sipendi kila mtu ajue"
"sikia dogo afu kwanza unaitwa nani?"
"naitwa sheby"
"hebu tupe namba ya simu coz tayari umeshakua mwenzetu wewe"
"aaa kwa bahati mbaya sina simu kwakweli"
"ila inatakiwa tudai haki zetu sheby. au unaonaje?"
"ni kweli ila ni kama nilivyokuambia kua mimi hua sipendi mtu anijue"
"sasa we wanakuridhishaje?"
"aaaa ninae mtu wangu spesho ambae namlipa"
"ila fresh pia kwaio sasa inakuaje? sisi ngoja tukuache au sio?"
"poa basi tutaendelea kuonana"
"poa bana sheby"
Niliachana nao pale maeneo walipokuepo

UNAJUA MASHOGA WA SIKU HIZI PIA WANAJAZIAGA MWILI, HIVYO NI HATARI KWA WEWE MWANAMKE UNAEJIFANYA UNAPENDA WANAUME WENYE MIILI YA MAZOEZI, NA MASHOGA WAPO WA AINA MBILI KUNA WALE WA KAZI KAMA KUIGIZA HIVI HUA NI LAZIMA UTAMKUTA ANA BODI KUBWA LA MAZOEZI UTAFIKIRI NI DUME LA SHOKA KWELI KUMBE NI SHOGA

NA KUNA HAWA AMBAO WANAJIUZA WENYEWE, HAWA HUA HAWANAGA MABODI MAKUBWA TENA NDIO KWANZA WANAJIWEKA KIDEMU DEMU.... SASA HAWA WALIOKUJA SASA HIVI MMOJA WAO YULE WA KWANZA NI WA KUJIUZA AFU WALE WENGINE WALIOKUA NA MABODI MAZURI YA MAZOEZI WALE NI SPESHO KWA KAZI ZA FILAMU NA NDIO MAANA WAKANIAMBIA KWANINI NISIUNGANE NAO NIKAPIGA PESA.

Sasa vile naachana na wale mashoga tu nilikutana na zaituni akiwa na gari yake, na alikua amenifata maana nyumbani hua wanatakaga saa mbili tu niwe nyumbani sasa leo nimepitiliza kutokana na hawa mashoga,
Zaituni alishuka kwenye gari na kuniuliza
"wale ni akina nani?"
"wale ni wachezaji wenzangu"
"muongo sheby hebu niambie ukweli coz wale wakaka mi nawajua vizuri tu"
"sasa si ndio nakuambia ni maplayer wenzangu?"
"hapana sheby hapa hunidanganyi kitu ng'oo coz wale wakaka ni mashoga wale"
"kwaio kama ni mashoga unatakaje?"
"sheby mdogo wangu ivi umzima kweli?"
"zaituni naomba sana tueshmiane"
"maskini sheby mdogo wangu usikute umeshajiunga kwenye kundi hilo wewe"
"sasa kwani inakuusu?"
"sheby ni kweli upo huko?"
"ndio kwani vp?"
Nilimuona zai akianza kulia huku akipanda kwenye gari kisha akaondoka kwa hasira......

Niliendelea kutembea zangu kwa mguu huku nikifanya mazoezi na usiku huo,
Nilifika nyumbani mida ya saa 2:30 nikamkuta zai keshafika nyumbani, sasa ile naingia tu ndani nilianza kupokelewa na zai huku akiniambia
"niseme kwa mama?"
"asa useme nini sasa?"
"si wewe na rafiki zako"
"acha unafki"
Niliingia zangu chumbani kwangu na kuelekea bafuni moja kwa moja nikaenda kuoga... Nilikua nafikiria sana kuusiana na dada zai kama atamuambia mama kwa vile alivyonikuta kule njiani na wale jamaaa, Nilimaliza kuoga nikatoka huku nikijipangusa maji na taulo
"heeeeeee asa nani kakuambia uingie chumbani kwangu bila hodi?"
"kwani una kipi ambacho sikijui?"
"zai? naomba tueshmiane sawa?"
"tuyaache hayo... ivi sheby? ivi ni kweli una hali hio?"
"kwani hata nikiwa nayo inakuhusu?"
"sasa si uniambie"
"sikuambii sasa"
Mara dada nusura alikuja kwa spidi kali
"nyie mnatupigia kelele bwana"
Aliongea hivyo kisha mimi nikamjibu
"mmmmnhhh dadaa yani kutoka huku juu hadi huko chini unasikia sauti zetu kweli?"
"amna si nilikua napita kutoka rumu ile kule"
"aaaaahhh nikajua ni kutoka huko chini"
"sasa mlikua mnagombana nini?"
"si hili li zai hapa"
"kafanyeje?"
"muuulize"
Nilikua naendelea kujifuta maji mwilini huku nikiwa nimevaa boxer, maana hata mimi mwenyewe saa mingine nawakutaga dada zangu wana taiti tu ila hakuna anaemuwaza mwenzie.. yaani malezi ambayo tumezoeshwa ni mabaya sana... coz naweza kwenda hata kwa dada nusura nikamkuta ana taiti lakini haniambiii toka nivae... bali bado wananichukulia kama mtoto mdogo vile. hivyo hata mimi wamenikuta natoka kuoga na boxer. ila siwawazii kua ni wanawake wala nini bali nawachukua kama dada zangu na wala sina wasiwasi.... ila hua kama yupo uchi kabisa ni lazima anifukuze au asiniruusu kuingia... ila chupi na taiti wananiruusu kuingia coz hata nikiingia hua sinaga tabia ya kumkodolea macho... yaani kifupi nakua kama vile nipo na mwanaume mwenzangu...

Coz kama ukiwa geto na mchizi wako.. afu akiwa anabadili nguo huoni haja ya kumuangalia. coz alichonacho ndio hicho we ulicho nacho hivyo hata hawa dada zangu ninapokua chumbani kwake hua naona kama vile nipo na mwanaume mwenzangu..... yaani sina lile wazo la kusema kua ngoja nimuangalie dada yangu kipapa chake au mapaja yake... au makalio yake.. yaani sina hata wazo la kumtamani kabisaaaaa....

Sasa hapa wote wamenikuta mdogo wao nina boxer tu. lakini pia wao hawana hilo wazo la kusema labda tumtupie mdogo wetu macho. yaani hata jinsi tunavyo ongea hua tunaongea utafikiri wote tuna nguo.. kumbe mmoja wetu yupo uchi.
"haya wewe zaituni ulikua mnapiga kelele za nini?"
"mdogo wa mgonjwa huyo"
"mgonjwa??? mgonjwa wa nini?"
"muulize si huyo hapo"
"Eti we sheby unaumwa nini kwani?"
"wala tu mbona siumwi kitu"
"sasa mbona mnanichanganya nyie?"
Tulikua kimya wote huku dada etu akiwa kakasirika ile mbaya, Maana hakuna anaetaka kusema
"we zai hebu niambie sheby ana nini?"
"mdogo wako mgonjwa huyo"
"sasa ni mgonjwa anaumwa nini?"
"nilimkuta leo njiani kasimama na wakina bakari shoga"
"heeeeee sasa kusimama nao tu ndio kosa?"
"we mteteee tu ila dogo lako sio rizki hilo"
"heeee we zai maneno gani hayo unaongea mbele yangu na kwa mdogo wako?"
"si tunamuambia ukweli"
"afu mbwa toka apa fala wewe"
Alimpiga kibao cha mgongo na kumtoa nje kisha akanirudia mimi.,..
"Ehee we sheby anachokisema zai ni kweli?"
"mmhhhh? hhhmm? hhhmmm? mmmmhh?"
"mmmnhhhhh nini hebu niambie nijue ili nikamuambie mama tukushuhulikie sheby"
"lakini dada?"
"sitaki kusikia lakini. bali niambie ni kweli una hali hio?"
"mmhhh waaapiii zai muongo tuuu"
"ila licha ya hivyo hata mimi nilishakutilia mashaka maana hupendi wanawake kabisa wewe"
"aaaaa sasa dada na wewe wataka uninyase nyase sio? sasa kama wewe na zai hali moja mi ndugu yangu ni nani sasa?"
"basi mdogo wangu.. mi mbona sikunyasi nyasi?"
"aaaa mmezidi kuniandama sana"
"pole basi.. au nisamee mimi basi sawa? haya vaa nguo basi"

Dada nusura nae alitoka zake huku akiwa na wasiwasi na mimi sana. ila mimi nilikua zangu Cool tu sina swaga na mtu. na huo uchafu wao wanaonibambikia mi siujui hata kidogo.

BAADA YA SIKU HIO KUPITA

Sasa leo ni juma tatu nikiwa najiandaa kwenda shule. nilioga kwanza kama kawaida yangu kisha nikavaa Uniform za shule.. huku nikiitwa na mfanya kazi kua chai tayari. Hua chai yangu inakuaga nzito kuliko zote....
Ghafla zai alikuja na kuanza kunywa chai pale meza moja na mimi..
"mambo?"
Alinisalimia kama kawaida
"poa"
"mbona kuitikia tu mpaka ujishauuueee?"
"kwani ni mdomo wako lakini?"
"lione vile... na nitamuambia mama tu"
"mwambie kwani inahuuu?"
"sawaaa"
Yaani mimi na zai tulikua hatupatanagi na sijui ni kwanini. maana tunaelewana dakika mbili na muda huo huo tunagombana tena... Zai aliondoka na kuelekea chumbani kwa mama.
Nikapiga zangu chai nzitoooo

Baada ya hapo nilichukua begi langu huku nikiwa na furaha binafsi kwa moyo wangu....

Sasa nikiwa napiga hatua ya kutoka nje ya geti nilishtuka kwa kusikia kelele za zaituni huko ndani.. zikiniita mimi
"shebiiiiiiii? we shebiiiii?"
"nini bwana mi nitachelewa school bus"
"mama ukuuuu"
"sasa kama ananiita kwanini asingeniambia toka saa hio bwana nyie?"
"bwana shebiiiiii mama kaanguka ukooo"
"kaanguka??? mungu wangu eee we zai utakua umemfanya nini mama?"
"mi sijui"
"muite dada nusura huko kwake"
Nilikimbizana na ngazi kuelekea chumbani kwa mama na kumkuta yupo chini hajiwezi kabisa
"mamiii? mamii ni nini kwani?"
"we sheby mamii kafanya nini?"
Aliniuliza dada nusura huku akianza kulia
"sasa unalia nini dada hebu kageuze gari vizuri... afu we zai njoo tumbebe basii"
"ah ah wewe zai kageuze gari vizuri wacha nimbebe na sheby fanya haraka"
Tulianza kua vichaa ndani ya muda mfupi huku nikiwa sina akili hata moja... Nilitupa begi la shule kisha tukaanza kumbeba mama etu..

HOSPITALINI

Tulikua tupo nje ya mlango wa wodi ambayo anafanyiwa matibabu. Siku hii ya leo wote mimi na zai hatukwenda shule kabisa.... tena zai alikua analia huku akiniangalia
"we sheby mama kafanyaje?"
"mi sijui ila alikua na zai ndani kule"
"we zai mama kafanyeje?"
"nilinaniiii?"
"ulinaniii? ulinanii nini sasa?"
Mara ghafla dokta kaja, tukaamka wote kwenye kiti na kumfata dokta
"dokta vp huko mamaa yupo sawa kweli?"
"cha kwanza naombeni niseme kua tumshukuru mungu kwa wema wake"
"doktaaaa hebu tuambie mamiii wetu anapumua au?"
"kijana kua mpole... ila kabla sijaeleza hali yake. kuna jambo kaniambia niwafikishie ninyi watoto wawili"
Tuliposikia tu hivyo nilimuona dada nusura akianza kutokwa na machozi
"dokta hebu niambie mamii wangu yupo katka hali gani?"
"kijana kua mpole... afu kaniambia nikupime wewe"
"afu we dokta falaas ninj wewe? yaani mi nakuuliza mambo ya mama angu afu unaniletea swaga za kupima hapa"
Nilijikuta nimekua mkorofi ghafla na kuishika lile likoti lake la kidokta na kulikata vifungo vyake...
"we mtoto mbona mkorofi wewe?"
"sema mama angu ana hali gani?"
"si uende ukamuangalie yupo mzima tuuuu.... yaani hii mitoto mingine sijui ipojeee?"
Niliingia ndani huku nikilengwa na machozi ya mbali
"mamiii shida ni nini mamiii?"
"mwanangu sheby"
Nilienda na kumkumbatia mama angu huku machozi yakimtoka kwa uchungu...
"mama hizo presha zilianza lini?"
"wala sio presha mwanangu... ila kuna kitu kaniambia dada yako zai"
Nilimuangalia zai kwa hasira hizo duu
"kwani kakuambia nini mamaa?"
"jamani mwanangu? ujue nakutegemea sana mwanangu"
"kwani kuna shida gani mama mbona mi nipo sawa tuuuu"
Mama alikua akilia kwa uchungu huku kama akinionea huruma....
"eti ni kweli una tatizo hilo mwanangu?"
"lipi hilo?"
"dada yako kuna jambo kaniambia kua una urafiki na wakina bakari.. na ndicho kilicho nidondosha na kupoteza fahamu maana mwanangu nakutegemea wewe"
Nilisubiri mama amalize maongezi yake huku akilia
"mwanangu? jua nami nahitaji mjukuu kutoka kwako mwanangu, vp eti ni kweli?"
Kwanza kabla sijamjibu niliamka moja kwa moja na kwenda kumkusanya zai hata kama ni dada yangu.....

Nilimkusanya na kumgongeza ukutani huku nikimpa mavibao ya maana kwa umbea wake
"we fala unataka uniulie mama angu kwa umbea wako sio? we fala si nakuuliza wewe?"
"bwana sheby niachie bwana iiiiiiiiiiiii iiiiiiiiiii uuuuuuiiiiiiiii"
Zai alianza kulia lakini nilimua wala simuachiii hata kidogo Ani nilikua nampa adabu nzuri kutokana na umbea wake.
Sasa mama alianza kupiga kelele kwa kuniita
"sheby muache dada yako sheby?"
Dada nusura nae alianza kutetea mpaka akashindwa kutuamulia...
"jamani nusura waamulie wadogo zako"
"we shebiiiiii? we sheby muache mwenzako jamani"
Nilikua mtoto wa kiume sisikii la muazini wala la mnadi swala....
"sheby mdogo wangu muache mwenzako utamuumizaaaa"
"jamani hawa watotoo"
"weeeeeee sadikiiiii muache mwenzio?"
Heeeeee wote tulishtuka kwa kusikia hilo jina la sadiki... Hata kumuadhibu zai niliacha na kumuangalia dada nusura kwa hilo jina alioliita
Hata mama mwenyewe alishangaa kusikia hilo jina... na hakutaka kulimezea mate kabisa.....
Mama alimuuluza dada nusura ambae ndio alitaamka hilo jina la sadiki
"we nusura? huyo sadiki ni nani?"

Bila LIKE yako hutoiona sehemu ya 11 hivyo

Prwss LIKE yako ili kuifanya iwe juu pia waruhusiwa kushare

USIKOSE KESHO KAMA MTAJAZA LIKE KUANZIA 50+

via #TeamDwacBoy

Ani ni #YediDay








Chagua kiongozi bora ili kuleta mabadiliko
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment