AFCON 2017: LEO NI LEO KUNDI G: TAIFA STARS v NIGERIA!


STARS-UTURUKI-MKWASABAADA ya kuchapwa 3-0 huko Misri katika Mechi yao ya kwanza ya Kundi G la AFCON 2017, Kombe la Mataifa ya Afrika, Tanzania, maarufu kama Taifa Stars, Leo wapo Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kucheza na Nigeria.
Nigeria, chini ya Kocha Sunday Oliseh, Mchezaji wa zamani wa Nchi hiyo, wao waliifunga Chad 2-0 katika Mechi yao ya kwanza ya Kundi G waliyocheza kwao.
Ili kujitayarisha kwa ajili ya Mechi hii, Taifa Stars walipiga Kambi ya Mazoezi huko Ulaya Nchini Turkey na Jana Kocha wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa, alisema wao wako tayari kwa mtanange huu.

+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
TIKETI:
-MAUZO:
-Vituo: (i) Ofisi za TFF - Karume , (iii) Mbagala – Dar live, (iv) Ubungo – Oilcom, (v) Makumbusho – Stendi, (vi) Uwanja wa Taifa, (vii) Mwenge – Stendi, (viii) Kivukoni-  Feri, (ix) Posta – Luther House, (x) Big Bon – Msimbazi Kariakooo
-Viingilio: VIP A Tsh 40,000, VIP B Tsh 30,000, VIP C Tsh15,000, Rangi ya Machungwa (Orange) Tsh 10,000, Rangi ya Bluu na Kijani Tsh 7,000.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
AFCON-KUNDI-G
Akiongea na Wanahabari Jana katika Ukumbi wa Mikutano wa TFF uliopo Uwanja wa Karume Jijini Dar es Salaam, Mkwasa amesema: “Tumefanya mazoezi kwa takribani siku kumi, vijana wako katika hali nzuri ya mchezo, uwezo waanaouonyesha mazoezini ni wa hali ya juu na unatupa matumaini ya kufanya vizuri”
TAIFA-MKWASA-PRESSPia Mkwasa alisema katika mpira hakuna kinachoshindakana na anatambua Nigeria ni Timu kubwa Afrika, waliotwaa Ubingwa wa Afrika mara tatu, lakini mpira wa sasa lolote linaweza kutokea na wao wamejiandaa vilivyo kufanya vizuri katika mchezo huo.
Mkwasa pia aliwaomba Watanzania kuja kuwapa sapoti Wachezaji Uwanjani kwa kuwashangilia muda wote wa mchezo.
Mechi hii itachezeshwa na Waamuzi kutoka Nchini Rwanda ambao ni Louis Hakizimana (Mwamuzi wa Kati) Honore Simba (Mwamuzi Msaidizi), Jean Bosco Niyitegeka (Mwamuzi Msaidizi), Abdoul Karim Twagiramukiza (Mwamuzi wa Akiba) na Kamisaaa wa Mchezo ni Charles Kasembe kutoka Nchini Uganda ambao wote tayari waliwaili Dar es Salaam tangu Juzi Jioni.
Mechi hii itaanza Saa 10 na Nusu Jioni, Saa za Bongo.
TANZANIA:
-KOCHA: Charles Boniface Mkwasa
-WACHEZAJI: lly Mustafa, Said Mohamed, walinzi Juma Abdul, Shomari Kapombe, Haji Mwinyi, Mohamed Hussein, Kelvin Yondani, Hassan Isihaka, Nadri Haroub “Cannavaro”, Himid Mao, Frank Domayo, Mudathir Yahya, Said Ndemla, Salum Telela, Deus Kaseke, Saimon Msuva, Farid Musa, John Bocco, Rashid Mandawa, Ibrahim Ajib, Thomas Ulimwengu, Mrisho Ngasa, Mbwana Samatta.
NIGERIA:
-KOCHA: Sunday Oliseh
-WACHEZAJI: Ikeme Onoro, Ezenwa Ikechukwu, walinzi Thomas Olufemi, Balogun Aderemi, kwambe Solomon, Omeruo Keneth, Ekong William, Oboroakpo Austin, Akasi Chima, na Madu Kingsley.
Wengine ni viungo Ibrahim Rabiu, Muhamed Usman, Uzochukwu Izunna, Haruna Lukman, Nwankwo Obiora, Igboun Emeka, washambuliaji Simon Daddy, Ujah Anthony, Emenike Chinenye, Musa Ahmed, Aggreh Obus na Eduok Samuel.
REFA: Louis Hakizimana (Rwanda)
+++++++++++++++++++++++++++++++
MECHI ZILIZOPITA:
06 Julai 1972 Tanzania 0 v Nigeria 0 [Kirafiki]
12 Januari 1973 Nigeria 2 v Tanzania 1 [African Games]
08Machi 1980 Nigeria 3 v Tanzania 1 [African Nations Cup]
06 Desemba 1980 Nigeria 1 v Tanzania 1 [Mchujo Kombe la Dunia]
20 Desemba 1980 Tanzania 0 v Nigeria 2 [Mchujo Kombe la Dunia]
11 Septemba 2002 Nigeria 2 v Tanzania 0 [Kirafiki]
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: