YANGA SC YAMUUZA SHERMAN MILIONI 300, ASAINI MIAKA MITATU MPUMALANGA BLACK ACESS

Habari za ndani zinasema Yanga SC italipwa dola za Kimarekani 150,000 (Sh. Milioni 300) kama ada ya uhamisho ya mchezaji huyo aliyesaini Jangwani kwa dola 60,000 (Sh. Milioni 120,000) Desemba mwaka jana.

Na Sherman aliyekuwa analipwa doka 3,000 (Sh. Milioni 6) kwa mwezi Yanga SC, sasa atakuwa analipwa dola 5,000 (Sh, Milioni 10) Black Aces kabla ya kukatwa kodi.
Kpah Sean Sherman baada ya kusaini Black Acess juzi

Mwenyekiti wa Aces, Mario Morfou ameiambia BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE kwa simu leo kwamba wanatarajia Sherman atakuwa pacha mzuri wa Mzambia, Collins Mbesuma katika safu ya ushambuliaji ya timu yake msimu huu.
“Ni mchezaji mzuri na mmoja wa wachezaji bora sana tuliowahi kusaini na sasa tunajivunia kuwa naye AmaZayoni,” amesema Morfou.
Sherman alijiunga na Yanga SCS Desemba mwaka jana akitokea klabu ya Cetinkaya ya Ligi Kuu ya Cyprus Kaskazini na katika kipindi hicho ameichezea timu ya Jangwani mechi 27 na kuifungia mabao sita kwenye mashindano yote.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miak 23 sasa, alianza kuichezea Cetinkaya mwaka 2012, akitokea Duzkaya SK aliyoanza kuichezea mwaka 
2010, akitokea Barrack YC ya nyumbani kwao, Liberia ambayo alianza kuichezea mwaka 2009

SORCE.BIN ZUBER
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: