Waziri wa zamani wa Elimu, Joseph Mungai
Waziri wa zamani wa Elimu, Joseph Mungai.
Waziri wa zamani wa Elimu, Joseph Mungai  ametangaza kukihama chama Chama Mapinduzi na kuhamia  umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).

Mungai ametangaza uamuzi huo katika mkutano wa hadhara wa kampeni za UKAWA  katika Uwanja wa Shule ya Msingi Wambi, wilayani Mufindi mjini Mafinga.
Mungai aliwahi kuwa mbunge kwa miaka 35 kupitia CCM na aliweza kuteuliwa nafasi mbalimbali za uwaziri ikiwamo Wizara ya Kilimo, Mambo ya Ndani na Wizara ya Elimu.
Katika mkutano huo Mungani alimnadi mtoto wake ambaye ni Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mafinga Mjini kupitia Chadema, William Mungai ambapo alisema wananchi wa jimbo hilo wanatakiwa kumchagua William Mungai kwa sababu mbunge aliyemaliza muda wake katika jimbo hilo hakuweza kuongoza kama alivyofanya yeye.
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: