Urais 2015: Zitto Kabwe azilipua CCM na UKAWA

Zitto Kabwe akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es salaam.
Zitto Kabwe akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es salaam.
Kiongozi wa ACT-Wazalendo Zitto Kabwe akizungumza katika mkutano wa mafunzo na chama cha hicho.
Kiongozi wa ACT-Wazalendo Zitto Kabwe akizungumza katika mkutano wa mafunzo na chama cha hicho.
Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe leo amewalipua chama cha Mapinduzi CCM pamoja na  Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kuwa  hawana jipya katika kinyanganyiro cha Urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika oktoba 25,2015.
Akizungumza na Waandishi wa Hababri leo  Zitto Kabwe amesema kwamba chama chake pekee ndicho kilichobeba ajenda ya kuwakomboa watanzania kutokana na  kuweka ajenda nne za msingi watakazozifanyika kazi endapo watafanikiwa kuchaguliwa kukliongoza taifa la Tanzania.
“Kama untaka siasa za Mbwembwe nenda CCM,Kama unataka siasa za ulaghai nenda UKAWA na kama unataka siasa za misingi siasa za issues ni ACT-Wazalendo” amesema Zitto Kabwe.
Amesema kwamba mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli katika kampeni zake anazungumzia hasa Barabara utadhani anakwenda kuwa Rais wa Barabara,  wakati   UKAWA wakiwa hawana jipya.
Chama chake kina ajenda nne ambazo
(i)Haki ya Watanzania kwenye hifadhi ya jamii kwa kupata bima afya,
(ii)Uchumi unaozalisha Ajira
(iii)Afya
(iv)Elimu
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: