Prof. Lipumba atangaza rasmi kujiuzulu Uenyekiti CUF

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahim Lipumba.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahim Lipumba.
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahim Lipumba leo ametangaza rasmi kujiuzulu wadhfa huo na kusema kuwa atabaki kuwa mwanachama wa kawaida.
Profesa Lipumba amesema uamuzi wake unafuatia kushindwa kuafikiana na makubaliano yaliyofikiwa na vyama vinne shirikishi vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Amesema hafurahishwi na kufanya kile wanachokifanya wenzake kwa kuwa atakuwa anakwenda kinyume na makubaliano ya uongozi bora.
Vyama vinne vinavyounda umoja huo ni CUF, Chadema, NCCR Mageuzi na National League for Democracy (NLD).

Profesa Lipumba 63, amekuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CUF kwa miongo miwili (1995 – 2015) na amegombea nafasi ya urais katika miaka ya 2000, 2005 na 2010
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: