Prof. Lipumba akana Kujiuzulu


Mwenyekiti wa CUF Prof Ibrahim Lipumba akizungumza na wanachama wa CUF.
Mwenyekiti wa CUF Prof Ibrahim Lipumba akizungumza na wanachama wa CUF.
Kufuatia kutokea sintofahamu iliyopelekea mkutano wa Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba na Waandishi  wa  Habari  kuahirishwa  hatimaye Prof. Lipumba amejitokeza na kukana kujiulu.

Katika mitandao mbalimbali ya kijamii kuanzia jana zimeenea taarifa kuwa Prof. Lipumba amejiuzulu suala lililopeleka leo kuitishwa mkutano na Waandishi wa Habari katika ofisi zao zilizopo Buguruni jijini Dar es salaam lakini  ghafla mkutano huo uliahirishwa.
Sababu ya kuahirishwa mkutano huo inadaiwa kuwa  ni wazee kumtaka Prof. Lipumba kuwaeleza kile alichopanga kuzungumza na waandishi wa habari huku wakiamua  kuitishwa kikao kati ya Prof. Lipumba na wazee wa chama hicho.
Akizungumza mara baada ya kufanya kikao na wazee hao Prof. Lipumba amesema kuwa hajajiuzulu  na kuwataka wanachama   kuhakikisha   kuwa  wanakijenga  chama  cha CUF.
Katika hatua nyingine wananchama mbalimbali  wa CUF wali izingira ofisi hiyo wakitaka kufahamu hatma ya kiongozi wao kutokana na kuwepo taarifa za kujiuzulu katika mitandao ya kijamii hivyo baada ya Prof. Lipumba kuzungumza nao wali ridhia na kuondoka katika eneo hilo la ofisi za CUF.
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: