Maelfu wajitokeza Ukawa wakizindua Kampeni

Wagombea Urais wa UKAWA Edward Lowassa na Juma Duni Haji.
Wagombea Urais wa UKAWA Edward Lowassa na Juma Duni Haji.
Maelfu ya wananchi  ya wananchi wamejitokeza katika uwanja wa Jangwani leo jijini Dar es salaam kushuhudia uzinduzi wa Kampeni za Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).
Uzinduzi huo umekuwa wa aina yake kufuatia kuwa na shamra shamra nyingi na za aina yake kuanzia jana siku ya ijumaa ambapo inadaiwa baadhi ya wananchi walilazimika kulala katika viwanja vya Jangwani kusubiri uzinduzi huo.
Akizungumza  katika mkutano huo  Mwenyekiti wa Chadema Freeman  Mbowe amesema kwamba wamezindua kampeni zao leo ili kuhakikisha kuwa wanawapa wananchi mabadiliko wanayo yataka ambayo yataleta maisha mapya kwa watanzania.
Amesema kuwa  umasikini sio sifa, wala wao katika umoja wa UKAWA hawatamani umasikini, wakati wa kuamini viongozi masikini hapana. wanataka Tanzania iondoke katika umasikini kwa sababu umasikini ni laana.
“Nimalizie kusema kwa nini Lowassa, sisi tulifanya tafiti, kwa sababu taifa letu limeendeshwa kwa propaganda kwa muda mrefu, Lowassa kwa muda wa miaka 10 amekuwa muhanga wa propaganda za CCM.”Amesema Mbowe.
Naye Fredirick Sumaye amesema   ametoka chama cha mapinduzi, katibu mkuu alisema wao ambao hawatukuteuliwa hatukuwa na maadili, amesema  kama kipimo cha maadili ni mheshimiwa Kinana yeye atakuwa  mtakatifu.
Amesema  leo Lowassa ametoka CCM ameonekana hafai, lakini ni Kikwete  ndiye  aliyemfanya waziri mkuu wake, kuna Rais anaweka kiongozi ambae hafai? Lakini ni Lowassa huyuhuyu ndiye aliyemuingiza Kikwete Ikulu.
Kwa upande wake mgombea Urais wa UKAWA  Lowassa amesema  sera yake  itakuwa  Kipengele cha kwanza elimu, cha pili elimu na cha tatu elimu. Maneno haya ameyaazima kwa waziri mkuu wa Uingereza. Cha kwanza elimu itakuwa inagharamiwa na serikali kuanzia darasa la kwanza mpaka chuo kikuu.
Eneo la pili la kilimo ili tuweze kutengeneza ajira za kutosha  na   eneo la   tatu  ni   kuweka  umuhimu afya iwe bora kwa akina mama na watoto wadogo.
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: