MABINGWA CHELSEA WAPOKEA KIPIGO KINGINE KWAO STAMFORD BRIDGE!

CHELSEA-STAMFORDBRIDGEMABINGWA wa England, Chelsea, wakicheza kwao Stamford Bridge huko London Mechi yao ya mwisho ya Kirafiki ya michuano ya International Champions Cup kabla Wikiendi hii kuanza kutetea Taji lao la Ubingwa kwenye Ligi Kuu England, wamefungwa Bao 1-0 na Fiorentina ya Italy.
Fiorentina, ambayo Juzi iliwabwaga Mabingwa wa Ulaya Barcelona Bao 2-1 katika Mechi ya International Champions Cup, waliingia Stamford Bridge wakiwa na Kikosi kilichobadilishwa Wachezaji 7.

Bao la ushindi kwa Fiorentina lilifungwa na Gonzalo Rodríguez katika Dakika ya 34 baada ya Kipa Begovic kulitema Shuti la Alonso na Rodriguez kumalizia.
Jumamosi, wakiwa hapo hapo kwao Stamford Bridge, Chelsea, ambao maandalizi yao hayakuleta matokeo ya kuridhisha baada kupokea vipigo kadhaa, wataanza utetezi wa Ubingwa wao kwa kucheza Mechi yao ya kwanza ya Ligi Kuu England kwa Msimu mpya wa 2015/16 na Swansea City.
VIKOSI:
Chelsea: Begovic, Cuadrado, Zouma, Terry, Aina, Mikel, Loftus-Cheek, Traore, Oscar, Moses, Falcao
Akiba: Courtois, Blackman, Ivanovic, Azpilicueta, Cahill, Matic, Fabregas, Ramires, Hazard, Willian, Remy
Fiorentina: Sepe, Rodriguez, Junior, Tomovic, Alonso, Vecino, Fernandez, Suarez, Roncaglia, Rebic, Babacar.
Akiba: Tatarusanu, Lezzerini, Hegazy, Bagadur, Badelj, Joaquin, Valero, Ilicic, Bernardeschi, Fazzi, Rossi

SORCE SOKA IN TANZANIA
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: