Maandamano ya Lowassa yapigwa marufuku Mbeya


Maandamano ya Lowassa jijini Dar es salaam.
Maandamano ya Lowassa jijini Dar es salaam.
Ikiwa saa kadhaa zimebaki kufanyika kwa mkutano wa  mgombea Urais wa Ukawa Edward Lowassa kuomba wadhamini jijini Mbeya, Jeshi la Polisi limetangaza kupiga marufuku maanadamano hayo.
Kwa mujibu wa barua ya  Jeshi la Polisi iliyotolewa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahmed Z.Msangi imepiga marufuku kufanyika maandamano na kuutaka UKAWA kufanya mkutano tu.

Katika barua hiyo  imewataka  wananchi kutofanya au kulazimisha maandamano yoyote yawe ya miguu au pikipiki. huku akisisitiza kuwa  ieleweke  si maandamano bali ni mkutano wa hadhara utakaofanyika katika viwanja hivyo. Kinyume na hapo hatua kali za kisheria zitachukuliwa.
Lowassa atawahutubia wananchi ikiwa ni katika mchakato wa kusaka wadhamini ikiwa ni moja ya sharti la Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC)  kwa wagombea wa vyama vyote kutafuta wadhamini katika mikoa kumi ya Tanzania bara.
Sifa za wadhamini ni pamoja na kuwa wamejiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura zoezi lililomalizika nchini kote siku kadhaa zilizopita
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: