LOWASA KUKUSANYA MAFURIKO KESHO


Mgombea Urais wa UKAWA Edward Lowassa.
Mgombea Urais wa UKAWA Edward Lowassa.
Waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa ambaye ni mgombea Urais kupitia UKAWA anatarajia kuwahutubia  wananchi   katika  viwanja vya tindigani kata ya kimandolu jijini Arusha siku ya jumamosi (kesho tarehe 15).

Akizungumza na Vyombo vya Habari Mwenyekiti wa chadema Mkoa wa Arusha Amani Golugwa alisema kuwa mapokezi hayo yamekamilika kwa asilimia mia moja. Lengo la ujio huo ni kumtambulisha mgombea urais ambaye ataambatana na mgombea mwenza Juma Duni Hajji.
Licha ya kumtambulisha   kwa wananchi wa Mkoa wa Arusha  pia  kwa ajili   ya  kupata udhamini wa huku  zoezi la udhamini likiwa  limeshaanza  mkoani  humo.
Baada ya mkutano huo kuisha msafara huo utaelekea katika jimbo la Monduli ambapo pia Mh.Lowassa atapata wasaa wa kuhutubia wananchi katika jimbo hilo.
Viongozi watakaokuwepo katika  msafara huo ni  Mwenyekiti wa Taifa Freeman Mbowe, wenyeviti wenza wa ukawa kutoka NLD, NCCR pamoja na chama cha CUF, John Mnyika, Nibu katibu mkuu Zanzibar Salum Mwalimu na viongozi wengine.
Amesisitiza kuwa  kwa   kushirikiana na jeshi la polisi pamoja na vikosi  vya usalama suala la Amani,Utulivu, Ulinzi na Usalama vitadumishwa katika msafara huo pamoja na mkutano huo.
Naye  Naibu katibu mkuu wa Timu Lowassa for president  Ndama Jeuri alisema wamejiandaa vizuri kumpokea  na wataendelea kuhamasisha watu kumuunga mkono Lowassa
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: