CCM yakanusha Magufuli Kugawia Laptop Walimu


Mgombea Urais wa CCM Dkt.John Pombe Magufuli.
Mgombea Urais wa CCM Dkt.John Pombe Magufuli.
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimekanusha vikali  taarifa  zilizo  enea katika mitandao ya kijamii kwamba mgombea Urais wa CCM Dkt.John Pombe Magufuli atawagawia Laptop walimu wote nchini Tanzania endapo akichaguliwa kuwa Rais.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es salaam leo Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye amesema kwamba Mgombea urais wa chama hicho hajawahi kusema kuwa atawagawia walimu laptop sehemu yeyote  ile.
Ameongeza kuwa taarifa hizo ni za upotoshaji na zimetolewa na wananchi wenye malengo mabaya kwa kuwa muda wa kufanya kampeni bado haujatangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yenye makao makuu jijini Dar es salaam.
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: