JESHI LA POLISI MKOA WA NJOMBE LIMESEMA MWENDOKASI NDIO CHANZO CHA VIFO VYA WATU 5 LUDEWA

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Wilbroad  Mutafungwa
 Kamanda wa Kikosi Cha Usalama Barabarani Mkoa wa Njombe Kelvin Ndimbo
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Wilbroad Mutafungwa Aliyekaa na Kamanda wa Kikosi Cha Usalama Barabarani[RTO]Kelvin Ndimbo Aliyesimama

Na Barnabas njenjema Ludewa

Jeshi la Polisi Mkoani Njombe Limesema Limebaini Chanzo Cha Ajali ya Gari Iliyosababisha Vifo Vya Watu Watano Wilayani Ludewa Kuwa ni Mwendokasi Aliokuwa na Dereva wa Gari Hilo.

Akizungumza na Vyombo Vya Habari Ofisini Kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Wilbroad Mutafungwa Amesema Kuwa Ajali Hiyo Iliyohusisha Gari Ndogo Yenye Namba za Usajiri T.613 AKA  Aina ya Toyota Cresta Imeanguka Kwa Kutumbukia Katika Mto Baada ya Dereva Ambaye ni Alon Haule na Mmiliki wa Gari Hilo Kushindwa Kumudu Gari Kutokana na Mwendokasi Aliokuwa Nao na Kisha Kutumbukia Mtoni.

Kamanda Mutafungwa Amewataja Waliokufa Kuwa ni Pamoja na ALONI HAULE (40) , PENDO MBAWALA (29) , WESLAUS MTWEVE (40) ,EDITHA HAULE (35) na PASCALIUS MLWILO (20) ambae ni mwanafunzi wa chuo cha Nursing Lugarawa.

Katika Tukio la Pili Kamanda Mutafungwa Amesema Jeshi la Polisi Mkoani Njombe Limepokea Taarifa Toka Kwa
Afisa Mtendaji wa Kijiji Cha Malimbuli Kata ya Mang'oto Wilayani Makete Alex Ponela Baada ya Kugundua Kuwepo Kwa Mauaji ya Joshua Salum Sudy Maarufu Kwa Jina la Mwaka Ambaye Amekufa Baada ya Nyumba Yake Kuchomwa Moto Kwa Wizi wa Kimapenzi.

Hata Hivyo Wito Umetolewa Kwa Watu Kuacha tabia ya Kujichukulia Sheria Mkononi na Kusababisha Madhara Makubwa ya Vifo na Uhalibifu wa Mali Katika Maeneo Yao Jambo Ambalo ni Hatari Kwao
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: