DR MAGUFULI AMPONGEZA FILIKUNJOMBEA AWAKUNA MLANGALI



MGOMBEA urais wa CCM Dr John Magufuli amempongeza mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe kwa kupita bila kupingwa huku akiahidi Neema kwa wakazi wa Mlangali kuwa ahadi Yake ya kwanza ni barabara ya lami na maji.

Mgombea huyo wa Urais alitoa kauli hiyo leo kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na wananchi wa Mavanga na kata ya Mlangali wakati wa kampeni zake za kutafuta ushindi wa CCM

Alisema kuwa shida za watanzania si vyama Bali kutatuliwa matatizo Yao na kuwa yeye atakuwa Rais wa vyama vyote bila kujali itikadi zao

Hivyo alisema iwapo ataingia ikulu kwanza kwa wakazi wa Ludewa ataanza na barabara ya Lami pia umeme wa uhakika na Huduma ya maji ikiwa ni pamoja na elimu bure kutoka shule ya msingi hadi sekondari kidato cha nne .

Alisema kuwa kikubwa anachojivunia kwa mbunge  wa Ludewa Bw Filikunjombe ni uchapakazi wake hivyo kwa pamoja wananchi wakichagua CCM kwa ngazi zote tatu ni uhakika maendeleo yatasonga mbele .

Dr Magufuli alisema kuwa akiwa Ikulu atahakikisha serikali Yake inakuwa na mawaziri watendaji wachapakazi na si vinginevyo 
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: