Aliyeshindwa ujumbe wa NEC Ludewa Eng. Zephania Chaula akiagana na mbunge Deo Filikunjombe baada ya kushindwa katika nafasi ya unec,
Ludewa ,, Wananchi wilayani Ludewa katika mkoa wa njombe wamelaani vikali kitendo cha mgombea Ubunge jimbo la Ludewa kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi (CCM)anayejulikana kwa jina la Zephania Chaula kukashfu na kutupia maneno ya matusi vyombo vya Habari ikiwemo Redio Best Fm Ludewa kuwa siyo Redio na kukiita kuwa ni Bad Redio.
Tukio hilo lilitokea julai 30 majira ya saa kumi jioni katika viwanja vya Soko la samaki ludewa mjini wakati wagombea watatu wa Ubunge kupitia CCM wakijinadi sera zao na kuomba kura kwa wananchi ambao ni Mh, Deo Filikunjombe anayemaliza muda wake wa uongozi kwa kipindi cha miaka mitano, Captain Mpangala pamoja na Zephania Chaula aliyetoa matusi hayo kwa chombo cha Habari cha Redio Best Fm Ludewa.
Akijibu swali la mwananchi aliyemhoji mgombea huyo mwenye matusi kuwa hivi karibuni vyombo vya habari viliripoti kuwa mgombea huyo alisema mara baada ya kukosa nafasi ya NEC kwa wilaya ya Ludewa alisema hata gombea Tena nafasi yoyote kupitia ccm Ludewa hivyo imekuaje Aombe kura kwa wananchi kupitia chama hicho na ndipo mgombea huyo alishindwa kijibu swali hilo na kuishia kuitupia lawama Taasisi ya Redio Best Fm kuwa imekuwa ikitangaza habari zake za kumkashfu kila wakati.
'' Asante bwana, Qula kwa kuniuliza swali zuri Najua kuwa hiyo ni Redio Best Fm mimi naweza kusema hiyo ni Bad Fm kwakuwa wamekuwa wakitangaza habari zangu za uchochezi kila wakati ili mimi nionekane Mbaya kuna siku mimi nitawapeleka mahakamani kwasababu redio hii inatoa habari za kichochezi kila wakati Alisema Mgombea huyo bwna Zephania Chaula''
Hata hivyo mgombea huyo mwenye matusi alisema kuwa anawaomba wananchi wa wilaya ya Ludewa wamuonee huruma kwakuwa amekuwa akiwania kiti hicho kwa zaidi ya miaka 10 hadi sasa na kukosa kauli ambayo imekanushwa vikali na mbunge wa Jimbo la Ludewa Mh, Deo Filikunjombe Ambae kwasasa anamaliza muda wake wa uongozi kwakipindi cha miaka mitano sasa na kusema kuwa kazi ya Ubunge si kazi ya utani na lelemama kwakuwa wananchi wa Ludewa Wanahitaji mabadiliko.
Mbunge Filikunjombe alikuwa wa mwisho kujinadi sera zake mbele ya umati wa wananchi wa Ludewa mjini na mara baada ya kumaliza muda wake wa kujinadi wananchi hao bila woga na bila kujali waliamua kuandamana na kumbeba mbunge huyo juu kwa juu na kuimba nyimbo za kumsifu mbunge huyo kwa kile walicho dai kuwa hakuna kama Deo Filikunjombe wa kuja kuwaletea mafanikio hivyo walisema Filikunjombe ni pekee na ndie watakae mtuma kwa mara nyingine ili kwenda kuwawakilisha bungeni.
Wananchi hao walisema kuwa wamechoshwa na kudanganywa na sera za wagombea ambao wamekuwa wakifika Wilayani humo hasa kipindi cha uchaguzi na kuomba kura bila ya kutoa mchango wenye mafanikio kwa wananchi wa Ludewa.
HAYO YANAFUATIA MARA BAADA YA,,,,,,,,, TUJIKUMBUSHE
MTANGAZA NIA UBUNGE LUDEWA ASHINDWA KUTWAA UJUMBE WA NEC, AAPA KUTOKUGOMBEA UBUNGE
Mkuu wa wilaya ya Ludewa Antonia Choya akimkabidhi Mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe (kushoto) hati ya shukrani ya kushiriki mbio za Mwenge.
Zoezi la kupiga kura likiendelea.
Mjumbe wa mkutano huo Bw. Choya akipiga kura
Wajumbe wakishiriki kupiga kura.
Wajumbe wakishiriki kupiga kura.
Chaula akishukuru kwa kushindwa.
Injinia Chaula akimpongeza mshindi mzee Nkwera.
Mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe akipiga kura kumchangua mjumbe wa NEC Ludewa
Mjumbe wa mkutano huo Bw. Choya akipiga kura
Wajumbe wakishiriki kupiga kura.
Wajumbe wakishiriki kupiga kura.
Chaula akishukuru kwa kushindwa.
Injinia Chaula akimpongeza mshindi mzee Nkwera.
Mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe akipiga kura kumchangua mjumbe wa NEC Ludewa
Aliyeshindwa
ujumbe wa NEC Ludewa Eng. Zephania Chaula akiangana na mbunge Deo
Filikunjombe baada ya kushindwa katika nafasi hiyo, Chaula alikuwa ni
mmoja wa wana CCM waliokuwa wakitaka kuwania ubunge jimbo la Ludewa.
Na MatukiodaimaBlog
MBIO
za ubunge jimbo la Ludewa mkoani Njombe zimeishia hewani kwa
mtangaza nia wa wanafasi hiyo Eng. Zephania Chaula baada ya
kuambilia kura 11 pekee katika nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri kuu (
NEC) Taifa kutoka wilaya ya Ludewa aliyokuwa akiwania dhidi ya katibu
msaidizi wa mbunge wa jimbo la Ludewa Hilaly Nkwera aliyeibuka
mshindi kwa kupata kura 138 kati ya kura zote halali 151 zilizopigwa
.
Huku
mgombea huyo aliyeshindwa katika nafasi hiyo ya Ujumbe wa NEC Injinia
Chaula akiapa kutogombea tena nafasi hiyo kwa madai kuwa ni mara ya
pili sasa anashindwa vibaya katika mchakato wa kuwania nafasi hiyo
ambapo awali alishindwa mgombea wa darasa la saba marehemu Elizabeth
Haule .
Uchaguzi
huo mdogo wa kuziba nafasi ya mjumbe wa NEC iliyoachwa wazi na
aliyekuwa Mjumbe wa nafasi hiyo Elizabeth Haule aliyefariki dunia
mapema mwaka huu ,ulifanyika mwishoni mwa wiki hii kwa
kuwashirikisha wagombea hao wawili kabla ya mgombea mwingine ambae
ni mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe kuandika barua ya
kujitoa katika kinyang'anyiro hicho akiwapisha wagombea hao
wachuane kutokana na yeye kudai kuwa atachukua fomu ya kugombea tena
ubunge wa jimbo hilo la Ludewa .
Akitangaza
matokeo hayo ya uchaguzi msimamizi mkuu wa uchaguzi huo Lucas
Nyanda ambae ni katibu wa jumuiya ya wazizi wa CCM mkoa wa Njombe
,alisema kuwa jumla ya wajumbe waliopaswa kushiriki katika
uchaguzi huo ni 164 ila wajumbe halali walioshiriki ni 151 na kati
ya wajumbe hao kura 2 ziliharibika huku Injinia Chaula akipata kura
11 na mshindi wa nafasi hiyo Bw Nkwera akipata kura 138
Awali mbunge wa jimbo la
Ludewa Bw Filikunjombe ambae alikuwa ni mmoja kati ya wana CCM
watatu ambao majina yao yalirejeshwa kuwania nafasai hiyo alisema
kuwa analazimika kujitoa katika nafasi hiyo ili kupisha wanachama
hao wawili ambao wamemzidi umri ili kuweza kupambana na yeye
ataendelea kuwa kuwatumikia wananchi wa Ludewa katika nafasi ya
ubunge pekee.
Akiwashukuru
wajumbe kwa ushindi huo wa nafasi ya ujumbe wa NEC Bw Nkwera ambae
kitaaluma ni mwalimu na pia amepata kuwa mwenyekiti wa Halmashauri ya
wilaya ya Ludewa na mwenyekiti wa madiwani wa mkoa wa Njombe na Iringa
alisema kuwa amefurahishwa na imani kubwa ambayo wana CCM wameionyesha
kwake kwa kumchagua kuwa mwakilishi wao katika vikao vya kitaifa .
Bw
Nkwera alisema wana CCM Ludewa waamini kuwa nafasi hiyo hawajakosea
kumpa na kamwe hatawaangusha kwani atahakikisha anawatumikia vema
katika vikao vya juu kwa kuanza na safari ya kumpata mgombea wa
nafasi ya Urais wa CCM ambae atakuwa ni chaguo la wana CCM wote wa
Ludewa .
Huku
Chaula mbali ya kuwashukuru kwa kura 11 alizopata bado alisema
kuwa hatakuwa tayari kuendelea kugombea tena kwani yawezekana kabisa
Mungu hajapenda yeye kuwa kiongozi wa kisiasa bali ametaka aendelee
kuwa mtaalam .
“Nasema
haya kutoka moyoni mimi ni mwanachama hai wa chama cha mapinduzi na
nakipenda chama change hivyo naahidi sitagombea tena katika maisha yangu
nafasi hii ya UNEC kutokana na ukweli kuwa nahisi siasa inanikataa
maana kila nikigombea nashindwa hivyo ngoja nifanye kazi nyingine pia
nampongeza sana mshindi Mzee Nkwera katika utendaji wake ndani ya
chama”,alisema Mhandisi Chaula.
Wakati
huo huo serikali ya mkoa wa Njombe kupitia mkuu wa mkoa wa Njombe
Dr Rehema Nchimbi imempongeza kwa kumpa hati ya shukrani mbunge wa
jimbo la Ludewa Bw Filikunjombe kwa ushiriki wake mkubwa katika
kufanikisha mbio za mwenge katika mkoa huo kwa kuwa mbunge pekee
kushiriki mbio za mwenge na kuchangia vizuri .
Akikabidhi
hadi hiyo mbele ya wajumbe wa mkutano wa Halmashauri kuu , mkuu wa
wilaya ya Ludewa Bw.Anatory Choya aliweza kumtunuku hati hiyo ya
heshima mbunge wa jimbo la Ludewa Filikunjombe kwa kushiriki kimamirifu
katika mbio za mwenge wa Uhuru ndani ya mkoa wa Njombe.
Akitoa
cheti hicho Bw.Choya alisema kuwa kutokana na ushiriki alioufanya
mh.Filikunjombe katika mbio cha mwenge wa Uhuru mkuu wa mkoa wa Njombe
na ofisi yake wameona wampatie cheti cha heshima Filikunjombe kwani ni
mbunge pekee aliyeshiriki katika mbio hizo za Mwenge katika mkoa wa
Njombe.
Barnabas njenjema Ludewa
0 comments:
Post a Comment