ONE DAY YES sehemu ya 8

Jivunie kuwa mwana ludewa















ONE DAY YES

Sehemu Ya 8

Mtunzi..... MoonBoy

Simu No. +255714419487 WhatsApp

Ilipoishia Jana ↓

"Eti we hadija?"
"nini?"
"unamjua yule jamaa pale?"
"jamaa gani wewe huku hakukaagi watu"
"jamani mtu si yule pale anatuangalia"
"yesu wangu kimbia wewe"

Sasa mfanyakazi alitupa ndoo ya mkaa na kukimbia... nami nikajaribu lakini nilishindwa kukimbia kwasababu ya mguu wangu na mkono hivyo nilibaki nikijiburuza tu chini kama paka aliokatwa kiuno... Sasa nikiwa najiburuza mara yule jamaa akatokea tena kwa mbele... Lakini nilipoiangalia hio sura ni kama naifahamu vile....

ENDELEAA



Nilikua ni muoga sana kwa wakati huo. maana nilitokewa na sura ambayo naifahamu kabisa. na sii mwingine bali alikua ni BABA YANGU MZAZI ndio alinijia. ila hakunifanya chochote zaidi ya kuniambia
"umekuja mjini? utapata shida sana mwanangu... kama kuna mtu alikuambia usije mjini ni bora ungelimsikiliza huyo mtu"
"kwani hakua ni wewe?"
"hapana sio mimi"
"na huyo mtu ni mwanamke au mwanaume?"
"mi pia sijui"
Alikua akiongea kabisa lakini nikimshika hashikiki kabisa. Ghafla alitoeka bila kujua kaondokaje hapo mbele yangu... lakini kidogo moyo ulikua na amani kwakua hakua mtu mbaya. Lakini pia nilikua nina wasi wasi kuusu ile stori alioniambia jamila japo hakuimalizia yote. Niliamka pale chini huku nikiwa na maumivu mengi sana katika mwili wangu. Nilipanda kitandani na kujipumzisha zangu maana nilikua naumwa na vile vidonda vya mguu

BAADA YA WIKI MOJA KUPITA

Na leo ni siku ya juma tatu asubuhi. Nilipiga zangu mswaki kisha nikawa namsubiri broo atoke ili niongee nae kuusu kazi.. maana namtegemea yeye kuhusiana na jambo hilo... Kweli punde si punde broo alitoka na kuwasha gari yake. nami nikamfuata kabla hajatoka getini hapo
"shkamoo broo?"
"marahaba vp?"
"poa tu"
"vp kuna tatizo?"
"Hapana hakuna tatio ila kuna kitu naitaji tu kukuambia"
"ni kitu gani hicho?"
"Aaaaa ni kuusu kazi broo.. kwan si unajua nimeacha familia hivyo naomba unifanye na mimi niwe na mchakariko wa hapa na pale"
"sasa familia yako inaniusu nini mimi?? kama umekuja mjini chakalika mwenyewe mzee hapa ni mjini"
"lakini broo si unajua mimi sina ninaemfahamu zaidi yako?"
"sasa skia, tena umeitibu kuanzia sasa hivi nakupa wiki moja tu ya kuwepo ndani ya nyumba yangu"
Aliongea hivyo kisha akaondoka zake kazini. nilibaki na maumivu tuu juu ya majibu yake Yani ni bora nisingemwambia,

Basi baada ya broo kutoka mara mkewe alitoka na kunikuta nimejiinamia pale pale nje. Alianza kuniongelesha mambo ya ajab ajabu tu
"we vp mbona umesimama hapa? Eheheeeeeeee halooo unajipendekeza kua ndugu wakati hamuna hata undugu loooo aibuuu"
"hapana shemeji ka"
"weeeeeeeeeee ukome na jina lako hilo.. toka lini nikaolewa na kaka ako?"
"huyu mtu huyu ni kaka angu kabisa na kama kakuambia kua hana ndugu basi huyo kakudanganya"
"mimi sinashida na kuzijua porojo zako hizo"
"lakini shemu mbona mi sina kisa na nyinyi lakini naona unanichukia tu bure"
"hebu nipishe mimi kinyago mkubwa wewe"
"mmhh sawa ila vp chai ipo?"
"chai? chai ipi hio? au ulipeleka mkundu pale kupika hio chai? au baba yako kaleta sukari huku ndani?"
"bac nisamee shemeji"
"nimesema hilo jina silitaki kwanini husikiii? ( paaaa...kibao )"
Alinipiga kibao cha mkononi tena mkono ule ule weye maumivu makali
"Aaaaaaiiiiiiiiii umeniumiza aisee"
"kufa kabisa mwana kidagala we.. mschiuuuuuu Usiojua ndugu na kuja kumng'ang'ania hatibu wangu...Eti hatibu ni ndugu yaaanguuuu nyooo"
Aliongea mengi sana kisha akaondoka na kuelekea saluni kutinda nywele...
Ghafla mfanya kazi alitokea na kuniinua pale chini niliposukumwa na shemeji...
"pole kaka"
"asante sana dada angu"
"ivi kweli ni ndugu yako huyu baba?"
"ndio ni ndugu yangu"
"mmhh pole sana kaka angu.. na vp umekunywa chai?"
"mnhh wala sijanywa dada angu"
"ok nenda kule ndani kwako nakuletea chai ila uinywe fasta fasta asije kuku kuta"
"naomba nisindikize basi maana nilivyosukumwa. niliutikisa huu mguu"
"usjali kaka angu"
Dada jamila alikua akinionea huruma sana. hivyo aliweza kunikokota hadi kule stoo kwangu ninapolala siky zote.
Baada ya kuniacha ghafla aliniletea chai na chapati.. nilianza kuzila haraka haraka na kuzifakamia kwa spidi ili nisije kukutwa na shemeji...
Nilichua dakika mbili tu kuimaliza chai ile. Basi hadija alichukua vyombo vyake na kufuta ushahidi wa kua nilikunywa chai...

BAADA YA SIKU MOJA KUPITA

na sasa ni mida ya jioni kama saa 10 hivi nilikua nimekaa sebuleni naangalia tv.. Mara jamila alikuja hadi hapo sebuleni
"eti we mkaka? kwanini usiongee na kaka yako kwa haya anayokufanyia shemeji yako?"
"mmhh dada angu.. kaka yangu mwenyewe yupo hivyo hivyo alivyo huyu shemeji... Kwasababu nakumbuka jana nilimuambia anifanyie mpango wa kazi Lakini sikuamini kwa majibu alionipa kwakweli"
"najua yatakua yamekuumiza sana hayo majibu"
"ni sana kuliko unavyofikiria"
Basi mfanya kazi aliondoka baada ya kuskia honi ya gari ikilia...
Nami nilikua na wasi wasi juu ya honi ile. maana kama ni shemeji basi nijijue kua nitakuja kugombezwa muda si mrefu. Nilikua nimetulia tu nacheki zangu filamu fulani hivi ya kibongo..

Ghafla shemeji alitokea pale sebuleni Na kuniangaliaaaa bila kupesha hata jicho...
"hee hee hee hee hee nani kakuruusu ukalie sofa zangu?"
"shkamoo?"
"kamuamkie baba ako kuzimu mbwa wewe shuka kwenye sofa zangu haraka"
Nilishuka fasta kwenye sofa za watu kisha nikakaa chini huku uwoga ukinijaa telee
"afu nani kakuambia uwashe tv?"
"nimewasha mwenyewe"
Nilidanganya ila aliewasha ni jamila hivyo nikakubali kosa.. mana siwezi kumsingizia mtu wa watu japo ni yeye ndio kafanya hilo kosa la kuniwashia tv...
"ushakua fundi na kichwa wa hii nyumba ee?"
"hapana shemeji"
"nyamaza mbwa wewe usiejua hata ndugu zako... mschiuuuuu ( msunyo )"
Mara jamila katokea na kumkuta shemeji akinisukuma na teke kwenye ule ule mguu unaouma
"dada usimfanye hivyo kaka wa watu"
"shiiiiii kimya na wewe... nitakugeuzia kibao wewe oohoo nadhani umenisahau wewe... kwanza nenda kwenye kazi zako"
Mara mlinzi nae alikuja huku akiwa kashikilia kirungu chake mkononi
"kuna nini hapa dada?"
"si huyu mwehu kaja kufungulia tv utafikiri ni kwake vile. mbwa huyu"
"lakini dada? huyu si ndugu yake na mzee?"
"ana undugu wapi huyu wala hawana hata undugu... usikute hata ni jirani yake tu"
"kwahio kumbe hana undugu?"
"hawana undugu hawaaa"
"eeeee makubwa"
Mtoto wa kiume nilikua nimetulia tu kimyaa sina nikianza kulengwa na machozi na kujuta kwanini nilikuja mjini.

Manyanyaso yalizidi kuwepo katika nyumba hii kila siku sikosi kuuziwa na shemeji. kwani nilikua kama nakomolewa katika nyumba hii. ila maisha ya ndugu ndivyo yalivyo hivyo sio cha kufanya kwani hata sasa hivi yenyewe nimepewa wiki moja tu. ya kuwepo hapa katika nyumba yake.

Sasa siku moja niliitwa sebuleni na nilihisi kutakua na kikao cha familia..Lakini cha ajabu nilimkuta shemeji analia kabisa na anaonekana kua na hasira na mimi. ila kwakua sikua na kosa lolote lile kwahio sikupaswa kuwa muoga juu ya hilo.....
"rashidi?"
Broo aliniita huku akiniangalia kwa hasira mno. na hapo ndipo woga uliponijaa teleee.
"ndio broo?"
"umekuja mjini kutafuta maishaa au umekuja kugombana?"
"kugombana? kugombana na nani?"
"unajifanya hujui?"
Nilikula kibao cha mbali mbali na kuanza kulia ghafla tu....... Na silii kwa maumivu ya kibao bali nalia kwa kusingiziwa jambo ambalo silifahamu kabisa...
"sijui kitu broo"
"umemfanyaje shemeji yako?"
"Eee mungu wangu... Eti shemeji nimekufanya nini mamii?"
Shemeji alianza kupayuka yote anayoyajua yeye kuusu nilichomfanyia... ila mi siui nimemfanyia nini kwakweli
"hatibu yaani huyu mtu wako ni wakuja kunitusi mimi? Yaani huyu kinyago wako ni mtu wa kunirushia mkono kweli? Siamini kama naweza kutukanwa na kugombezwa na kinyago kama huyu.. na usipoliangalia hili mimi narudi zangu kwetuuuu"
Alikua akiongea huku akilia kwa uchungu kuashiria ni kweli nilimtukana lakini sio kweli
"haaaaaaaaaa shemeji mbona mi sijakufanya chochote mamii?"
"nimesema hivi? usipolifanyia kazi mimi naondoka zangu kwetuu"
"hapana mke wangu.. hawezi kukufanya uondoke bali yeye ndio aondoke ila sio wewe...... rashidi? sasa nasema hivi kachukue kila kilicho chako na uondoke zako ulipotoka"
"broo broo sasa na usiku huu ndugu yangu nitalala wapi kaka?"
"mimi sitaki kujua hizo shida zako... kwanza ulikuja mikono mitupu.. kwahio naomba unyooke getini haraka"
"kaka naomba unisamee kaka sintorudia tena"
Niliomba msamaha kwa kosa ambalo hata silifahamu kabisaaa...
Daaahh mtoto wa kiume leo ndio nimeamini kweli ndugu sio wa kuishi nao na hawana msaada wowote... na sio kila mwenye ndugu mjini ana maisha mazuri bali wengine tunavumilia tu.. kwani hata hayo mateso sikuanza leo. lakini nimevumilia hadi nimefikia kufukuzwa katika nyumba za watu.. Nilitoka moja kwa moja huku nikiwa na mguu wangu wa tatu ( magongo ) Nilifunguliwa geti lakini mlinzi nae roho ya huruma pia ilimjia ghafla tu
"mmhh ndugu yangu kiukweli sina cha kukuseidia ila chukua hii elfu 10 na hili koti langu vikuseidie tu ndugu yangu... na naomba unisamee sana kwani mateso yako ni tuu mach kwakweli"
"usijali kaka tupo pamoja na nakushukuru kwa huruma yako"
Sasa kabla sijatoka nje mara jamila nae kaja huku akiwa muoga muoga
"chidi? nakuombea tu ufanikiwe huko uendako kwakweli ila mimi sina cha kukupa zaidi ya huu mshahara wangu wote nakupa wewe na chukua hiki kitenge kitakuseidia hata kujifunika chidi.. uende salama"
Jamila alinipa shilingi Elfu 30 ambao ni mshahara wake alioupokea juzi tu...
"nami nashukuru sana kwa ukarimu wenu nami naami mungu hatoniacha peke yangu"
Sasa nikiendelea kuwashukuru mara ghafla niliskia sauti ya broo
"kuma mayo bado hujaondoka tuu?"
Nilitoka mbio baada ya kuskia hivyo ila imeniuma roho kwa kutukaniwa mama yangu... ila sijali yote ni maisha tu... na naamini ipo siku na mimi nitatusua tu...... Daahh nilikua nipo hapo getini nikiendelea kufikiri pakwenda..
Niliangalia tu juu ya mbigu na kuongea neno moja tu
"ONE DAY YES"
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: