SERIKALI YAPIGA MARUFUKU WAKULIMA WILAYANI LUDEWA KULIMA MAENEO YA MAKAZI YA WATU

ninakuhabarisha kutoka ludewa njombe tanzania

baadhi ya wakazi wilayani ludewa wakiwa katika shughuli za kilimo moja ya maeneo ya mjini licha ya kupigwa mafuku


 NA BARNABAS NJENJEMA,
LUDEWA ,NJOMBE
Baadhi ya wananchi wilayani ludewa mkoani Njombe, wamelalamikia kitendo cha serikali yao ya halmashauli wilaya ya ludewa , kutoa kauli ya kutolima karibu na makazi yao, kwa kile walicho kiita kuwa hawana mashamba, na umri wao wengine ni wazee hivyo hawawezi kulima mashamba ya mbali.

Wakizungumza na njenje news blog,wananchi hao walisema kuwa, serikali ingetoa kauli hiyo kwa kuwaangalia, kwa kuwa haijawatendea haki hasa wazee, ambao hawanauwezo wakwenda umbali mrefu, kwa kuwa maisha yao ni magumu.

Hata hivyo walisema kuwa ,kwa mda mrefu wamekuwa wakiishi kwa shida kutokana na ugumu wa maisha ambao upo wilayani hapa hasa kwa wazee, ambao wamesema hawana msaada wowote ule jambo ambalo wameomba liangaliwe kwa ukaribu.

Aidhaa wameiomba serikali yao kuwaangalia kwa karibu, kwa vile sasa ni msimu wa kilimo,  kwani kuna mambo mengi ambayo yamekuwa yakitokea msimu huu kipindi cha masika.

serikali ya halmashauli wilayani hapa ilitangaza kuwa ni marufuku kwa wananchi kulima karibu na makazi yao hasa mazao yanayokuwa marefu kama mahindi,mtama n.k

lengo la kutoa kauli hiyo ni kuepukana na baadhi ya maovu yanayotokea katika kioindi hiki cha masika ikiwa pamoja na ukabaji wa watu hasa nyakati za usiku  pamoja na kuweka mazingira ya mjini kuwa safi muda wote..
 



Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: