Ngoma ya Mganda Yatawala Mashindano ya Umoja Tarafa ya Masasi
Ngoma ya asili ya Mganda ni miongoni mwa ngoma maarufu za jadi inayopatikana kusini mwa Tanzania, hususan katika mikoa ya Njombe, Ruvuma, na maeneo ya Ludewa, ikiwemo Tarafa ya Masasi na Tarafa ya Mwambao.
Ngoma hii ina asili kutoka kwa makabila ya Wangoni, Wamanda, na Wakisi. Wachezaji wake huvaa mavazi ya kitamaduni, yakiwemo masafi na nguo nyeupe pamoja na viatu vyeusi — vinavyowakilisha heshima, nidhamu na asili ya jamii hizo.
Katika kata ya Luilo, tarehe 19 na 20 Julai 2025, kulifanyika mashindano ya ngoma ya Mganda kwa lengo la kuimarisha umoja na mshikamano wa jamii. Zaidi ya maboma 11 yalishiriki, kila moja likiwasilisha ujumbe wa kijamii kupitia uchezaji wa ngoma hiyo ya asili.
Kama ilivyo desturi yao, Boma la Liagule liliendelea kuonyesha umahiri mkubwa kwa kucheza ngoma hiyo kwa maringo, ustadi na ujumbe mzito, na hatimaye kuibuka mshindi wa kwanza. Hii hapa orodha ya maboma yaliyoshiriki na nafasi walizopata:
Matokeo ya Mashindano:
1. Shujaa na Liagule
2. Liyombo, Iwela, Paradiso na Ludewa Mseto
3. Amani ya Litumba, Nkinilila, Nkomang'ombe, Idusi na Litumba Muungano
4. Staff Makali, Lifua na Ndongosi
Mashindano haya si tu yalitoa burudani, bali pia yalithibitisha umuhimu wa kudumisha utamaduni na sanaa ya asili kwa kizazi cha sasa na kijacho.
0 comments:
Post a Comment