KITUO CHA MABASI SONGEA KUFUNGULIWA LEO

KITUO cha Mabasi cha Songea  mjini kinatarajiwa kufunguliwa Septemba 7 mwaka  huu . katika kikao cha wadau  wa usafirishaji  ambacho kimefanyika  leo na kuongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dk.Mahenge,wadau hao wa usafirishaji wamepitisha kwa pamoja kuwa Stendi  ya Songea mjini itatumika kwa ajili ya daladala zote ambapo kituo cha Mabasi cha Msamala  kitatumika kwa ajili ya Mabasi yote yanayosafiri  nje  ya Mkoa wa Ruvuma  na yanayosafiri  ndani ya Mkoa wa Ruvuma. Stendi ya Mabasi ya Songea mjini in a uwezo wa kukaa Mabasi 96 na daladala 29 ambapo  Stendi ya Mabasi ya Msamala in  uwezo wa kukaa Mabasi 112 ,daladala 212 na Mabasi mdogo 84.Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amemwagiza Mkurugenzi wa manispaa ya Songea kuanzia Septemba 7 kuanza kutoza ushuru katika Mabasi, daladala,taksi na toroli katika stendi ya Songea mjini.Tayari kitengo cha TEHAMA kimeshaingiza kwenye mfumo  viwango vya tozo vitakavyotumika ambapo Mabasi ya Mkoa sh.3000,Mabasi ya wilaya sh.2000,daladala sh.1000,taksi ndani ya Stendi sh.3000, gari ndogo binafsi sh.500  na toroli sh.500




Ludewa yetu na maendeleo yetu posted by barnabas njenjema, kutoka Ludewa
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: