BEST FAMILY YACHAPWA NA MADINDO FC KATIKA MSIMU WA LUDEWA AMSHA MICHEZO 2016

Yaliyojiri katika mechi ya kirafiki baina ya timu ya watangazji wa kituo cha redio best family na timu ya kijiji cha madindo fc kutoka kata ya ludewa.

katikati ni katibu wa mbunge wa jimbo la ludewa Ndg.Fungatwende kushoto ni timu kapteni wa Best family salum mohamed a.k.a fundi kulia ni meneja mkuu wa redio best fm ludewa wakiteta jambo kabla ya mechi 


mashabiki wa timu ya madindo fc wakishangilia ushindi wao



katibu wa mbunge akisalimiana na wachezaji wa best family ya ludewa



katibu akisalimiana na timu ya madindo fc


Mtangazaji wa kituo cha redio best fm ludewa Nicksoni mahundi pamoja na meneja mkuu wa best fm mshairi wakimkaribisha mgei rasmi ambaye ni katibu wa mbunge wa jimbo la ludewa Ndug fungatwende

picha ya pamoja ya vikosi vya mpira wa miguu best family na mdindo fc 


katibu wa mbunge akitoa zawadi ya jezi kwa timu ya madindo fc



Katika harakati za kukuza michezo mbalimbali  katika wilaya ya ludewa uongozi wa Radio Best fm Ludewa kupitia katika kipindi cha best sport kinacholuka kila siku kuanzia sa 2 kamili hadi saa 3 kamili usiku kwa pamoja wameunda kikosi cha mpira wa miguu ambacho kinacheza mechi mbalimbali za ndani na nje ya wilaya ya Ludewa ambao unakwenda kwa jina la msimu wa amsha amsha michezo 2016.
juma pili hii timu hiyo ya watangazaji wa radio best fm ilishuka dimbani kucheza na timu ya kutoka katika kata ya ludende kijiji cha madindo.
mchezo huo ulikuwa mzuri na wakuvutia mashabiki walio furika katika uwanja wa halmshauli ya wilaya ya Ludewa hadi dakika tisini zinamalizika best family walikuwa wamechapwa magoli mawaili wa moja.
katika mchezo huo mgeni rasmi alikuwa ni katibu wa mbunge jimbo la Ludewa Ndg.Fungatwende aliyetumia nafasi hiyo kuwaasa vijana kupenda michezo ili kuepukana na vitendo viovu.
pia ndug Fungatwende licha kuwapongeza madindo fc kwa mchezo mzuri na wenye Nidhamu na kutoka na ushindi katika mechi hiyo dhidi ya best family  alioa zawadi ya jezi set moja kwa timu ya madindo fc.
lakin hakuwa mbali kukisifu chomba cha habari cha redio best fm ludewa kwa kuwa mstari wa mbele katika kukuza michezo  na kuendeleza michezo mbalimbali katika wilaya ya Ludewa
ikumbukwe ni msimu wa Amsha Amsha 2016 redio Best fm Ludewa inazunguka katika vijiji mbalimbali ili kukuza na kuendeleza michezo mbalimbali katika wilaya ya ludewa

2016 tupo karibu yako


 Ludewa yetu na maendeleo yetu posted by barnabas njenjema, kutoka Ludewa
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: