NEEMA YA UJENZI WA BARABARA NJOMBE MBIONI KUJA





 Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe Mohamed Ally
 Waziri Professa Mbalawa Akiwapungia Mikono Wananchi wa Kijiji Cha Usalule Wilayani Wanging'ombe Mkoani Njombe



 Diwani wa Kata ya Ulembwe Agnetha Mpangile Akishukuru Hotuba ya Waziri Mbalawa


 Meneja wa TANROADS Mkoa wa Njombe Yusuph Mazana Mwenye Koti la Kijivu Akiwa na Waziri Makame Mbalawa wakati wa Kikagua Barabara ya Njombe Makete

Na Barnabas Njenjema NJOMBE;

Waziri wa Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa Amesema Serikali Imetenga Kiasi cha Shilingi Trioni 4. Kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 Kwa Ajili ya Kutekeleza Miradi ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Barabara Pamoja na Usafiri wa Majini Anga na Reli  .

Katika Mazungunmzo Yao na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dkt. Rehema Nchimbi , Profesa Mbarawa Amemueleza Mkuu Huyo wa Mkoa Kuwa Katika Fedha Hizo Zitatumika Katika Ujenzi na Ukarabati wa Barabara za Mkoa wa Njombe Zikiwemo zaNjombe  Makete, Itoni  Ludewa Mpaka  Manda , Barabara ya Makambako Mbeya na Pamoja na Barabara ya Kibena Lupembe Hadi Madeke.

Awali Akizungumza na Kujibu Baadhi ya Hoja za Wafanyakazi Pamoja na Wakuu wa Idara Zilizochini ya Wizara Hiyo Profesa Mbarawa Amewataka Watendaji Hao Kufanyakazi Kwa Uadilifu , Huku Akiwashauri Wafanyakazi Hao Kujiendeleza Kielimu.

Mapema Wakitoa Malalamiko Yao Mbele ya Waziri Huyo wa Ujenzi ,Uchukuzi na Mawsiliano Baadhi ya Wafanyakazi Wameelezea Kufanya kazi Kwa Muda Mrefu Bila ya Kupewa Ajira ya Kudumu Licha ya Kuwa Uzoefu wa Kutosha na Badala Yake Wamekuwa Wakifanyakazi Kwa Mkataba wa Muda. 

Waziri Mbarawa Amefanya Ziara ya Siku Moja ya Kukagua Baadhi ya Miundombinu ya Barabara Pamoja na  Kuzungumza na Watendaji wa Taasisi na Idara Zilizochini ya Wizara ya Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano na Kutoa Maagizo Kwa Watendaji Hao.

Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Professa Makame Mbalawa Akielekea Dodoma Baada ya Kuhitimisha Ziara Yake Mkoani Njombe


Ludewa yetu na maendeleo yetu
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: