Nape ahimiza maudhui ya ndani kwenye vyombo vya habari





Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo Nape Nnauye .
Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo Nape Nnauye .

Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo Nape Nnauye  amevitaka vyombo vya habari kuhakikisha kuwa maudhui ya vyombo vya habari yanakuwa kwa asilimia kubwa ya ndani ya nchi.
Akizungumza  na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) kwenye hafla ya kuwakaribisha wajumbe wa Kamati ya Maudhui  katika ukumbi wa makao makuu ya  TCRA  Nape amesema vyombo vya habari vinatakiwa kuzindatia maudhui ya ndani kwa asilimia zaidi ya 60  tofauti na hali halisi ilivyo ya asilimia 60 ya maneno ambayo siyo vitendo.
Amesema kumekuwepo na malalamiko mengi kutoka kwa wadau ikiwemo wasanii kuwa vyombo vya Habari vinazingatia kwa asilimia kubwa maudhui ya nje suala linalopelekea wao kukosa mirabaha.
Naye kiongozi wa maudhui ya utangazaji TCRA Fredrick Ntobi amesema kwamba kwa sasa Mamlaka hiyo inafanya  kazi kubwa katika kuchunguza maudhui ya vyombo vya habari na kuvichukulia hatua vyombo ambavyo vinafanyakazi chini ya asilimia 60
Ludewa yetu na maendeleo yetu
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: