Mchungaji Peter Msigwa Apandishwa Mahakamani Kwa Kuwajeruhi Polisi

MGOMBEA Ubunge jimbo la Iringa Mjini kupitia Chadema, Mchungaji Peter Msigwa na wenzake watatu, wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Iringa wakituhumiwa kushambulia na kujeruhi askari polisi wawili.
 
Katika mashitaka hayo, Msigwa ambaye alikuwa Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini na Waziri kivuli katika Wizara ya Maliasili na Utalii katika bunge lililopita, alifikishwa na wenzake watatu shitaka linalowakabili washitakiwa 10 kwa makosa hayo.

 Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Blandina Manyanda aliwataja washitakiwa wengine waliofikishwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu Makazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Iringa, David Ngunyale, kuwa ni Edwine Sambala(66), Joseph Mgima (56) na Josephat Chengula (36).
 
Manyanda alisema kuwa washitakiwa hao walitenda makosa hayo Septemba 28 mwaka huu, ambapo watuhumiwa hao kwa pamoja walifanya makosa hayo kwa kufanya kosa la uvunjifu wa amani katika eneo Sambala Kata ya Gangilonga na kuwasababishia usumbufu kwa watumiaji wa barabara ya Iringa Dodoma.





Chagua kiongozi bora ili kuleta mabadiliko
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment