Nini Hatma ya Dr. Slaa UKAWA ?


Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa.
Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa.
Sintofahamu imeendelea kugubika ndani ya Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA kuhusiana na Hatma ya Katibu mkuu wa Chadema  Dr. Wilbroad Slaa aliyetofautiana na chama hicho kufuatia Mwanasiasa Edward Lowassa kupewa ridhaa ya kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe hivi karibuni aliwaambia wafuasi wa Chadema na Ukawa kwa ujumla kwamba  kumekuwepo na kutokuelewana kati ya Katibu Mkuu ambaye ni Dr.Slaa pamoja na Wanchama wa Chama hicho kutokana na ujio wa Lowassa.
Mbowe alinukukiliwa akisema Chama cha Chadema hakiwezi kuwa chama cha kuhubiri mabaya ya jana na kuacha kujadili maendeleo ya kesho,hivyo kama kuna mtu hakubaliani na maamuzi ya chama hicho akae pembeni atafakari kwa kina kwa maslahi ya Chama na Taifa kwa ujumla.
Licha ya Kauli hiyo Hivi karibuni Dr. Slaa alisema kwamba  muda utakapofika atazungumza kila kitu hivyo kuwataka wananchi na wanachama kusubiri uamuzi huo.
Katika hatua nyingine Dr. Slaa ameweka kauli tata kupitia ukurasa wake wa Twita zinazozua minong’ono katika jamii huku baadhi  ya  wanachi  wakisema kwamba huenda Dr.Slaa akabwaga manyanga kama ilivyotokea kwa Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Lipumba aliyetangaza kujiuzulu na kutimkia nchini Rwanda kufanya utafiti wa maendeleo.
Wakizungumza na mtandao wa Hivisasa baadhi ya wanachi na wanachama wa UKAWA wameonekana kutofurahishwa na maamuzi hayo ya Dr.Slaa kukaa pembeni  huku wanachama wa CCM wakiwaombea njaa UKAWA kama ambavyo ule msemo wa “adui yako muombee njaa” unavyotanabaisha.
Hizi ni baadhi no 3 no 1 ya kauli za Dr.Slaa,…
aw2 kajy no 1 no 3
Kutokana na kauli hizo nini hasa hatma ya Dr.Slaa Chadema pamoja na UKAWA kwa ujumla? Mimi na wewe hatujui hebu tusubiri kama alivyoa ahidi muda ukifika  ataweka wazi msimamo wak
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: