Chama cha Demokrasia na
maendeleo (Chadema) na vyama washirika vinavyounda umoja wa katiba ya
wananchi (UKAWA ) wamesema kuwa wako imara na wamejiandaa vyema kushinda
katika uchaguzi mkuu ujao kwa kukiondoa madarakani chama cha mapinduzi,
licha ya kauli inayodaiwa kutolewa na katibu mwenezi wa chama hicho
Nape Nnauye wakati wa ziara ya katibu mkuu wa chama hicho mkoani Mwanza
kwamba CCM itashinda hata kwa goli la mkono.
Kauli hiyo imetolewa
katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya magomeni
kirumba jijiji Mwanza na kuhudhuriwa na maelfu ya wananchi wa mikoa ya
kanda ya ziwa ambapo katika mkutano huo mwenyekiti wa taifa wa Chadema
Mh.Freeman Mbowe amewatambulisha rasmi waliokuwa wabunge kwa tiketi ya
chama cha mapinduzi Mh. James Lembeli na Mh. Esther Bulaya ambao
wamehamia Chadema, huku akiwatahadharisha wagombea wa nafasi za udiwani
na ubunge kutokubali kununuliwa kwa lengo la kukihujumu chama hicho.
Awali mwenyekiti wa
taifa wa baraza la wanawake wa Chadema (BAWACHA) Halima Mdee, naibu
katibu mkuu wa chama hicho upande wa Zanzibar Salum Mwalim pamoja na
mwanasheria wa Chadema Tundu Lissu wamesema wakati umefika kwa
watanzania kuchagua viongozi wanaokubalika na wenye uchungu na raslimali
za taifa kwa uhuru bila kutishwa kwani saa ya ukombozi kupitia sanduku
la kura utajulikana oktoba 25 mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment