CHADEMA yatoa ruksa kwa Mwanasiasa yeyote kuhamia

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willbrod Slaa.
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willbrod Slaa.
Chama Cha Demokrasia na Mendeleo kimesema kuwa  mtu yeyote ana uhuru wa kuhamia chama chochote cha Siasa ili mradi wafuate kanuni na taratibu  suala linalotoa ruksa kwa wanachama wengine kuhamia katika chama hicho.

Akizungumza  na Wananchi leo Mkoani Mwanza  mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe amesema kwamba  kupanda kwa gharama za maisha kumetokana na serkali iliyopo madarakani huku akitolea mfano kuwa mwaka 2010 wananchi waliweza kununua kilo ya Nyama kutokana na maisha yalikuwa chini ila hivisasa bei ya vitu iko juu.
Naye Katibu Mkuu wa Chama hicho Dk .Wildroad Slaa amesema kwamba  Chama cha Mapinduzi kimewapokonya wananchi serikali yao na kuifanya kuwa ni ya watu wachache na kuwataka kuichagua Chadema ili iweze kuwarudishia wananchi serikali yao ilipokwa kwa muda mrefu.
Katika mkutano huo Chadema imewatabulisha wanachama Wapya ambao ni Ester Bulaya pamoja na James Lembeli.
Chama hicho pia kimewataka wananchi kuwa wapole kwani kinatarajia kumtangaza mgombea wake wa urais mwezi  agosti tarehe 4 huku kikisisitiza kuwa hakifanyi mambo eti kwa vile chama fulani kimefanya.
Hivi karibuni kumekuwa na tetesi kuwa Mbunge wa Monduli Edward Lowassa naye ni  mmoja wa wanasiasa wanaotaka kuhamia katika chama cha Chadema kufuatia jina lake kukatwa katika kinyang’anyiro cha urais kilichofanyika wiki moja iliyopita ambapo Dk.John Pombe Magufuri ameibuka kidedea. Lakini hata hivyo hajaweza kuthibitisha madai hayo.
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: