ULIZIONA PICHA WAKATI MWENGE WA UHURU UKIWASHWA JANA HUKO SONGEA ? ZIKO HAPA


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akiwasha Mwenge wa uhuru jana mjini Songea katika Uwanja wa Majimaji ikiwa ni sehemu ya sherehe za uzinduzi wa mbio za Mwenge kwa mwaka 2015
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akihotubia jana mjini Songea wakati wa sherehe za uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa uhuru zilizofanyika kitaifa mkoani Ruvuma.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein (kushoto)akimkabidhi  Kiongozi wa Wakimbiza Mwenge Kitaifa Juma Khatibu Chum (kulia)  Mwenge wa uhuru jana mjini Songea baada ya uzinduzi wa mbio hizo Kitaifa mkoani Ruvuma.
 Kiongozi wa Mbio za Mwenge kwa mwaka 2015 Juma Khatibu Chum(kushoto) akimkabidhi  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu(kulia)  Mwenge wa uhuru jana mjini Songea baada ya uzinduzi wa mbio hizo Kitaifa mkoani Ruvuma.
 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu(kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Songea Profesa Norman Sigalla King(kulia) Mwenge wa Uhuru uhuru kwa ajili ya kuanza mbio wilayani humo baada ya uzinduzi ulifanywa jana mjini Songea  na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akihotubia jana mjini Songea.
Wananchi wa Mji wa Songea na Vijiji jirani na Mji huo wakiwa katika uwanja wa Majimaji Mkoa wa Ruvuma kushuhudia uzinduzi wa mbio za  Mwenge wa Uhuru Kitaifa uliowashwa na  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein

Maafisa mbali mbali wakiwa katika uzinduzi wa Mbio za mwenge kitaifa uliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein leo katika Uwanja wa  Majimaji Songea Mkoa wa Ruvuma

Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: