Boko Haram kuiga mfano wa Islamic State

Kiongozi wa kundi la wapiganaji wa Boko Haram nchini Nigeria ametoa taarifa akiahidi kuliheshimu kundi la wapiganaji wa Islamic state.Abubakr Shekau alitoa tangazo hilo katika ujumbe wa sauti uliowekwa katika mtandao,ambapo aliwaagiza waislamu wengine kuiga mfano wake.Islamic state Haijulikani ni vipi muungano huo utakuwa lakini mwandishi wa BBC katika eneo la mashariki ya kati anasema ni propaganda za kundi la Islamic State ambalo limekuwa likishindwa katika makabiliano nchini Iraq na Syria. Kundi la wapiganaji wa Boko Haram limetekeleza mashambulizi kadhaa kwa lengo la kutaka kuweka utawala wa kiislamu kazkazini mwa Nigeria ambapo maelfu ya watu wameuawa. -BBC Swahili
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: