CHOMBEZO RAHA ZABODA BODA sehemya 3

Ilipoishia;;;;; Kadiri spidi ya pikipiki ilipozidi, yeye alimlalia suka mgongoni na kukaza mikono kumkumbatia na hali hiyo pia ilimfanya akwepe manyunyu ya mvua na kuhisi kajoto f’lani hivi… Alijikuta akipeleka mikono hadi kuanza kushikashika flaizi… “Hee!” Suka alipiga ukelele wa uendawazimu wa kidereva wa bodaboda… KOKOTANA NAYO… “Nini tena jamani?” aliuliza Mage baada ya kelele za dereva huyo… “Si huko unakokwenda,” alisema suka. Mage akabaini haraka sana kwamba alishika sehemu isiyostahili kushikwa bila ruhusa na bila kuwepo kwa uhusiano. “Ooo! Samahani sana mwaya,” alisema Mage. Mvua ilichanganya kiasi kwamba, ilibidi dereva huyo aendeshe bodaboda polepole na kwa umakini wa hali ya juu. Mage ili kujificha na mvua ilibidi amwegemee zaidi dereva eneo la mgongoni huku mikono yake akizidi kuikaza kwa kumkumbatia asije kudondoka… “Hapo mbele ingia kushoto,” alielekeza Mage huku akizidi kumkumbatia kwa sana… “Hapo mbele kata kulia…pita kwenye hicho kibanda.” Mvua ikawa ya radi sasa, tena nzito. Ilibidi waegeshe bodaboda nje ya duka lililofungwa kwa usiku huo… “Da! Mvua kubwa sana,” alisema Mage. “Sana. Sijui nitarudije mimi?” “Itakatika,” alisema Mage na kweli muda huohuo mvua ilikata ghafla lakini Mage alishafika kwake kwani kwenye duka walilosimama na kwake ni nyumba tatu tu… “Naomba namba yako suka maana kesho nina safari f’lani hivi nitataka unipeleke wewe,” alisema Mage. Suka alitoa namba zake za simu, Mage akazisevu huku akisema… “Nimegundua wewe ni dereva mzuri, unajitambua. Nitakuwa nakutumia kwenye safari zangu mbalimbali maana mimi naogopaga sana kupanda bodaboda… “Hata pale Magomeni uliponishauri namna ya kukaa nikasema huyu ana akili sana, anajali abiria wake,” alisema Mage akiondoka baada ya kulipa. *** Kulikucha, Mage alichelewa kuamka kwa sababu ya kuchelewa kulala. Mdogo wake ndiye aliyetangulia kuamka na kufanya usafi. Mage alipoamka alifikia kukaa sebuleni… “Joy, huwezi kuamini jana kwa mara ya kwanza nimepanda bodaboda mwenzako.” “Kurudi?” “Eee…mpaka hapo nyumbani kwa mama Masuke. Lakini yule dereva yuko makini sana, anajitambua,” alisema Mage… “Kweli dada! Mimi si nilikwambia bodaboda hazina shida.” “Kweli kabisa.” *** Saa kumi na moja jioni, Mage alikuwa na safari ya kwenda Magomeni, akampigia dereva wake… “Eee…uko wapi?” “Nipo Biafra, nani mwenzangu?” “Mi yule dada wa jana usiku uliyenileta Kimara.” “Oo! Niambie…” “Njoo unichukue, nakwenda Magomeni.” “Poa.” Dereva aliondoka na bodaboda yake lakini huku akiwa na maswali mawili-matatu kuhusu akili za Mage… “Sasa huyu dada labda kama pesa inamuwasha. Kuita bodaboda iliyopo Kinondoni kwenda kumchukua Kimara impeleke Magomeni, haiingii akilini hata kidogo.” Baada ya dakika ishirini, bodaboda ilisimama nje ya duka la jana yake usiku,akampigia simu… “Haloo kama upo nje nakuja, namalizia kuvaa,” alisema Mage na kukata simu bila hata kusubiri jibu la kweli alikuwa amefika nje au pengine dereva huyo alitaka kubatilisha safari. “Da! Nimekuweka kweli jamani,” alisema Mage akipanda na kukaa mkao uleule wa jana yake usiku. Alishafundishwa kwa hiyo alipopanda tu,akamkumbatia dereva… “Duu!” dereva aliguna moyoni Kwa jinsi alivokumbatia . Safari ikaanza. Mage kama jana usiku, alimlalia mgongoni dereva lakini safari hii si kukwepa manyunyu ya mvua bali upepo mkali.Njiani walikokuwa wakipita, watu walimkodolea macho Mage kwani kaa yake ilikuwa ina mvuto wa aina yake. Mbaya zaidi alijaliwa wowowo la nguvu halafu blauzi aliyovaa ilipanda juu na kuacha sehemu kubwa ya kiuno kilichopambwa na cheni nzuri ya Gold kuonekana murua, ikaonekana pia chachandu na ‘kufuli’ rangi ya Pink. Vijana wa kihuni walipigia miluzi. Alimwelekeza suka sehemu ya kuingia na kwamba ameshafika… “Sasa saa hizi sikulipi, nitakupa usiku ukija kunichukua,” alisema Mage baada ya kushuka. “Sawa, utanipigia,” alisema suka. Mage aliendelea na mambo yake mpaka saa tatu usiku, akampigia simu dereva wake… “Niko tayari, nifuate mara moja.” “Sawa.” Dakika tano nyingi, bodaboda ikawa imefika… “Kumbe hukuwa mbali,” alisema Mage akitanua miguu kupanda pikipiki hiyo. Alipokaa sawa akapeleka mikono kumkumbatia suka kama kawaida, safari ikaanza. Kwa usiku huo, Mage hakuwa na wasiwasi kama mchana ambapo alificha sura ili wanaomjua wasimwone kwamba amepanda bodaboda. Kwa usiku huo alikuwa akiangalia sehemu mbalimbali huku wakati mwingine akijiegemeza kichwa kwenye mgongo wa dereva. Barabara ilikuwa nyeupe kwa hiyo dereva aliongeza mafuta zaidi na hivyo kumfanya Mage azidi kumkumbatia sana. Mage alijisahau na kuanza kushikashika sehemu ya flaizi kwenye suruali ya suka huyo. Safari hii suka hakusema neno kama jana yake usiku. Mage alipoona ni amani,akaanza kufungua zipu, kichwa akikiegemeza zaidi mgongoni na kusinzia kwa mbali… “Huyu demu ananitaka, we mwache tu,” suka alisema moyoni mwake. Mage alipoona jamaa hasemi neno, akaingiza mkono taratibu huku akijilamba midomo yake kama mtu mwenye msisimko baada ya kulamba kipande cha limao……………………… ITAENDELEA WIKI IJAYO…
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: