PHIRI AWAAMBIA WACHEZAJI WAKE MAANA YA MARADUFU NA KAZI ZAKE

Jivunie kuwa mwana ludewa



Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Phiri amewataka wachezaji wake kutoamini ushindi wa mchezo mmoja, badala yake kujiandaa upya kila baada ya mechi moja.


Phiri amesema kikosi chake kinaanza kuonyesha mabadiliko tofauti na ilivyokuwa awali, lakini suala la kujituma halikwepeki.

Akizungumza na SALEHJEMBE, Phiri amesema kila baada ya mechi moja ni maandalizi ya mechi nyingine.

"Ukishinda moja, unaanza kuwaza nyingine. Ushindi mmoja haukamilishi kila kitu au sare au kupoteza mara moja, hakupotezi kila kitu.

"Nazungumza sana na wachezaji pamoja na wasaidizi wangu, wanajua haya ninayokuambia.

"Simba ni timu kubwa sana na kila mmoja angefurahi kuiharibia, kila anayejua anakutana na Simba, maandalizi yake yanapanda maradufu.

"Sasa kwa mchezaji aliye Simba, maandalizi yake yanatakiwa kuwa maradufu kila siku kwa kuwa kila mechi ni dhidi ya walioajiandaa maradufu," alisema Phiri.

Tayari Simba iko kambini Zanzibar kujiandaa na mechi yake ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Kagera Sugar.

@salehe jembe
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: