KALOU AINGIA KWENYE MAZOEZI YA YOGA, MWANADADA AMBEBA JUUJUU
Mshambuliaji wa Hertha Berlin ya Ujerumani, Salomon Kalou amekuwa akifanya mazoezi ya kipekee wakati wa mapumziko haya ya baridi.
Kalou aliyewahi kung’ara na Chelsea, yuko New York, Marekani akishiriki mazoezi ya aina ya Yoga.
Taarifa nyingine zimeeleza kwamba anaweza kuyatumia mazoezi hayo kwa vichwa vya kuchumpa.
Kalou raia wa Ivory Coast amekuwa akifanya mazoezi hayo kwa kumshirikisha kaka yake pia.
Yoga humsaidia mtu kupumzisha mwili, lakini ni mazoezi yanayofanya mwili wa mhusika kuwa laini na lahisi kujikunja kwa kila namna.
0 comments:
Post a Comment