i wish you happy chrismass and happy new year
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Jimbo la Korogwe Mjini, kimeanza kuwashughulikia waliokuwa wanachama wake baada ya kudai kuwa ni virusi kwa kukikosesha ushindi katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika Desemba 14, mwaka huu.
Miongoni mwa waliotimuliwa ni pamoja na waliokuwa wagombea katika uchaguzi wa serikali za mitaa kwa mwaka huu nchini na kusababisha Chadema kupata kura sifuri katika jimbo hilo.
Miongoni mwa waliotimuliwa ni pamoja na waliokuwa wagombea katika uchaguzi wa serikali za mitaa kwa mwaka huu nchini na kusababisha Chadema kupata kura sifuri katika jimbo hilo.
Kwa mujibu wa Katibu wa jimbo hilo, Ezekiel Mbwilo hatua hiyo ni moja ya chama hicho kujisafisha kwa kuwatimua wanachama wake 42 miongoni mwao wakiwamo waliokuwa wakiwania uongozi kwenye uchaguzi huo kwa tuhuma za kukihujumu chama.
Mbwilo alisema Kwamsisi wametimua wanachama sita, Mahenge (10), Kitifu (25) na Manundu kati ni aliyekuwa mgombea wa uenyekiti anayedaiwa kurubuniwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) hivyo kujitoa dakika za mwisho.
Alisema kutimuliwa kwa wanachama hao muda mfupi baada ya kumalizika kwa uchaguzi huo kumetokana na kugundulika kwa baadhi yao kukihujumu chama kwa kupewa hongo na wapinzani wao.
Akizungumzia kuhusu uchaguzi huo, Mbwilo alisema uligubikwa na mizengwe na uwazi kutokuwepo huku misingi ya haki ikikosa kuzingatiwa.
Mbwilo alisema Kwamsisi wametimua wanachama sita, Mahenge (10), Kitifu (25) na Manundu kati ni aliyekuwa mgombea wa uenyekiti anayedaiwa kurubuniwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) hivyo kujitoa dakika za mwisho.
Alisema kutimuliwa kwa wanachama hao muda mfupi baada ya kumalizika kwa uchaguzi huo kumetokana na kugundulika kwa baadhi yao kukihujumu chama kwa kupewa hongo na wapinzani wao.
Akizungumzia kuhusu uchaguzi huo, Mbwilo alisema uligubikwa na mizengwe na uwazi kutokuwepo huku misingi ya haki ikikosa kuzingatiwa.
Na Dege Masoli -NIPASHE
0 comments:
Post a Comment