AUAWA KWA KUCHOMWA KISU NA HAWARA YAKE MDOGO HUKO MOROGORO

Mkazi wa Wilaya ya Kilombero,Morogoro Amon Nyenja amefariki dunia baada ya kuchomwa na kisu na anayedhaniwa kuwa ni hawara wa mke wake mdogo. Ofisa Mtendaji wa kata ya Mang’ula Shabaan Lichaula na Mkuu wa kituo cha Polisi Nkilijia Lazaro walisema Polisi inamshikilia mwanamke huyo ambaye ni mke wa marehemu wakati wakimsaka mtuhumiwa. Lichaula alidai marehemu katika kumtafuta mkewe alimkuta amesimama mahali na mwanaume huyo na baadaye mwanamke huyo alikimbia na kutokomea na marehemu kuamua kumvaa mgoni wake lakini alizidiwa baada ya mtu huyo kumchoma kisu cha ubavuni hadi utumbo kutoka nje. Alisema baada ya marehemu kuchomwa kisu alipiga kelele za kuomba msaada na wasamaria wema walijitokeza na kumwahisha hospitali na alifariki dunia baada ya kufanyiwa huduma ya kwanza wakati akihamishiwa katika hospitali Mtakatifu Fransis,Ifakara kwa matibabu zaidi. @eddy blog
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: