AGGREY MORRIS ASEMA HUU NDIYO WAKATI MSUVA AENDE ZAKE ULAYA

Beki wa kati wa Azam FC, Aggrey Morris, amemvulia kofia kiungo mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva na kusema kuwa hakabiki kirahisi ni bora atimkie Ulaya kwani uwezo wa kucheza anao. Beki huyo alimwaga sifa hizo baada ya kumalizika mchezo wa Ligi Kuu Bara kati ya timu yake na Yanga ulioisha kwa sare ya mabao 2-2 ambapo Msuva alionekana mwiba kutokana na kusumbua ukuta wa Azam uliokuwa chini ya Serge Wawa na Morris. Mchezo huo ulipomalizika mashabiki wa Yanga walionekana kuikubali timu yao licha ya matokeo hayo kutokana na kiwango kizuri kilichoonyeshwa na timu hiyo inayonolewa na Kocha, Mdachi, Hans van Der Pluijm. Beki huyo anayecheza ‘kazikazi’ alisema mchezaji aliyempa wakati mgumu katika mchezo huo ni Msuva licha ya uwepo wa mastraika wa kigeni Mliberia, Kpah Sean Sherman pamoja na Mrundi, Amissi Tambwe. “Mchezaji mzuri ni yule anayejua kukaa katika ‘position’ mzuri, mastraika wa Yanga wamecheza vizuri, hasa yule Mliberia na Tambwe ingawa hawakunipa shida sana. “Kwangu aliyenisumbua ni Msuva, jamaa anajua sana, yani akikupita tu basi, kinachotakiwa ni kumalizana naye haraka anapokuwa na mpira. Ninafikiri ana uwezo mkubwa anaweza kucheza soka hata Ulaya akipata nafasi,” alisema Aggrey
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: