Rais wa Nigeria atoa neno kuhusu soko la watu





Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari amesema raia wote wa Nigeria ambao wamekwama Libya watarejeshwa nyumbani na kusaidiwa kurejelea maisha ya kawaida kwani nchini humo wamekuwa wakiuzwa kama Mbuzi.
Tokeo la picha la buhari
Muhammadu Buhari
Akizungumzia video za karibuni ambazo zimekuwa zikiwaonesha Waafrika wakiuzwa kwenye mnada wa watumwa nchini Libya, Rais Buhari amesema inasikitisha sana kuona “baadhi ya raia wangu wa Nigeria wanauzwa kama mbuzi kwa kiasi cha dola kadhaa nchini Libya”.
Ameonekana pia kushangaa iwapo raia wa Libya walijifunza lolote la maana tangu kuondolewa madarakani kwa Kanali Muammar Gaddafi mwaka 2011.
Walichojifunza pekee ni kuwapiga watu risasi na kuua. Hawakujifunza kuwa mafundi wa umeme, mafundi wa mabomba au ufundi wowote ule,” amesema Buhari.
Kwenye video iliyotolewa na CNN mapema mwezi huu, vijana kutoka mataifa ya Afrika kusini mwa jangwa la Sahara walionekana wakiuzwa kama wafanyakazi wa mashambani kwa wanunuzi.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Buhari ameapa kupunguza idadi ya raia wa Nigeria wanaolazimika kufunga safari ndefu na hatari kupitia jangwa la Sahara na bahari ya Mediterranean kufika Ulaya.
Chanzo : BBC


Ludewa yetu na maendeleo yetu posted by barnabas njenjema, kutoka Ludewa




Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: