CHOMBEZO; HEHEE, KANTANGAZEEE!!! SEHEMU YA NNE


MTUNZI; IBRAHIM GAMA



Akafungua biashara hii ambayo bado haijaenea sana mjini inayolipa sana.
Mtu kufanyiwa Massage kila kiungo kina bei yake. Mtu mmoja mzima kummassage inafika hadi shilingi laki moja.
Ninatoka nafikiria nakwenda wapi sasa kwani nishaharibu kila kitu changu kwa siku moja tu. Nikiwa natembea kwa miguu mdogomdogo mara simu yangu inaita. Natazama namba ya simu inayopiga naona jina la SHEMALE kwenye kioo cha simu.
Ninaiacha simu yangu inaita zaidi ya mara tatu, ninaipokea huku nikiwa nimenuna sana, kwani Nisomtaka yuhoi, ninomtaka hana habari nami.
“Halow Dobe hapa.”
Ninaitikia kwa unyonge nimenuna balaa.
“Dobe pole sana mpenzi wangu, sasa nataka kujua hapo ulikuwa ukilipwa shilingi ngapi kwa mwezi?”
SHEMALE ananiuliza akiwa hana hata chembe ya utani kwenye maneno yake.
“Pale nilikuwa nalipwa pesa ndogo tu, laki moja kwa mwezi, hivi ninavyoongea na wewe nimesimamishwa, au sijui nishafukuzwa hiyo kazi yenyewe wala sijui. Nimeambiwa niende nyumbani hadi nitakapoitwa, haya hapo kuna kazi tena?!”
Ninajibu huku ninamaliza kwa swali nikiwa nimekata tamaa sana.
“Pole sana, usihofu mpenzi wangu, mie nimekupenda sana, kwani una Uume nzuri ambao naweza kupigia show wala nisiumie. Pia unajua sana kumuandaa mtu. Hebu nikuulize, unaweza kuendesha gari?”
SHEMALE ananizidisha uchungu ila yeye hajui tu, kwani bila yeye mie nisingekuwa mitaani hivi sasa.
“Mie dereva na leseni ninayo, je kuna pahala panatakiwa dereva?”
Ninamjibu huku nikiwa na shauku kubwa sana.
“Mie nataka nikuajiri utakuwa ukiniendesha, nakulipa elfu hamsini kwa wiki, na ukinipa mambo yangu nakupa laki moja kila mwezi, yaani nitakuwa nakulipa shilingi za kitanzania laki tatu kwa mwezi, je unasemaje upo tayari uanze kazi hata saa hii?”
Kwa kweli kazi sina, ninahitaji sana kazi ili maisha yaendelee. Ingekuwa kumuendesha peke yake tu, ningekubali haraka sana hata sasa, lakini hili la pili la kumuingilia, hapana moyo wangu unakuwa mzito.
Huu mtihani sana kwani nae ana jinsi inayosimama ipo siku atanambia na mie anigeuze kwa ajili ya nyege na pesa zake! Hapana sitaki kabisa kugeuzwa mie. Mwanaume rijali siwezi kuwa na tamaa namna hiyo.
“Nimekuelewa naomba unipe muda wakufikiri.”
Ninamjibu huku nikiwa sina nia ya dhati kufanya kazi kwake, natambua atanishawishi tu nicheze nae michezo yake michafu.
“Dobe unajifikiria kufanya kazi, wakati huna kazi?! Ama kweli asie bahati habahatiki. Kumbuka wapo watu wengi wanatafuta kazi, hivyo kama unaipiga teke riziki shauri yako, utakuja kuitafuta usiipate. Huko kufikiri kwako nikupe siku ngapi kwani nataka kufanya maamuzi.”
Ninafikiri kabla sijamjibu, hatimae namwambia
“Nipe kama wiki mbili hivi nitakuwa nishapata maamuzi sahihi.”
SHEMALE anaangua kicheko kikubwa sana, kisha ananambia kwa kejeli.
“Haya mzee wakufikiri. Yaani wewe ndiyo mtanzania wa kwanza nakusikia kuhusu kupewa kazi unataka kwanza ufikirie. Haya bwana fikiri ila mie naona shetani wako hapendi pesa. Unawachezea watu pale kazini kwako na kuwatia bila hata kukulipa pesa. Lakini pia unalipwa mshahara mdogo sana wa shilingi laki moja kwa mwezi. Mie nataka niwe nakulipa pesa nyingi unasema unajifikiria! Haya kaka Dobe endelea kufikiria ila unaitupa bahati. Wapo watu wengi wanaililia bahati hii hawajaipata. Haya ongea na shemeji yako huyu anataka kukusalimia.”
Mara naisikia sauti ya kike ambayo haina furaha
“Halow shemeji hujambo?”
Nasita kuitikia kwani sauti ninayoisikia siyo ngeni masikioni mwangu.
“Halow shem mbona kimya jamani hujambo?! Mie shemeji yako naitwa Njasi.”
Moyo unanienda mbio kama saa mbovu. Yaani huyu SHEMALE keshanitangaza tayari! Nikiwa bado nimenyamaza ninasikia kicheko kikubwa kutoka upande wa pili. Sauti ya Jesca ikisikika kwa sana.
“HEHEE, KANTANGAZEE!!! Na risiti tunakupa.”
Siwezi tena kuvumilia, ninaikata simu yenyewe, kisha naizima kabisa.
Ninafura kwa hasira yaani Jesca keshanitangaza tayari. Sijui na Njasi nae kantangaza! Yaani kama Jesca ndiyo kanitangaza kwa Njasi basi hakika amezidi kunibomolea kila pahala, kuanzia kazini kwangu hadi kwa mtu ambae ameuchukua moyo wangu wote.
Ninashindwa kujua ukweli wa hayo ninamua niende zangu nyumbani nikapumzike kwani kichwa chote kimevurugika. SHEMALE, JESCA ameniharibia siku, kazi yangu pamoja na mpango wa kando.
Ninafikiria nimpigie simu kisha nimtukane aachane na mimi, naliona hilo bado siyo wazo bora kwani hawa watu wa jinsi hizi, wana kamusi za maneno machafu vinywani mwao, wala siwawezi kabisa.
Watu hawa hawana haya wala hawajui vibaya. Ninaamua kukausha mikausho mikali.
Natoka sinza kazini kwangu naenda home Tabata Segerea. Ninapofika Home, hata njaa siisikii, kabisa nimechoka kila kitu, ninaamua kujitupa kitandani kama mzigo, nagalagala kwa mawazo usingizi unanipaa!

********
Siku ya pili naamka home mapema kama kawaida yangu ninavyoamka siku zote kwa kwenda kazini, lakini nabaki nimekaa kitandani. Lindi la mawazo limenitawala. Kazi yangu naiona ipotea kama wimbi la mto Ruvu. Sina raha kabisa kwani maisha haya yakurudi Salon wakati mie wanajua nalipwa mshahara mzuri kwa kazi yangu, kumbe hakuna lolote, lakini pia nimesimamishwa na kazi yenyewe basi naona aibu kwenda kubangaiza jambo la jana kwa leo.
Naona nifanye subira, kwani mungu si Athumani, lolote laweza kutokea ukimuamini yeye. Ninaichukua simu yangu naiwasha, kwani tangu nilipoizima jana sijarudi hewani tena.
Baada ya simu kuwaka mara ninapokea ujumbe kwenye mfululizo. Ninaziangalia moja baada ya moja, nakutana na ujumbe kutoka katika namba ngeni. Unanivutia zaidi. Ninausoma kwa makini kisha ninaamua kuiuliza jina la mmiliki wa namba hiyo katika mtandao wa Tigo, kwa Tigopesa.
Ninapolitazama jina lake moyo wangu unanienda mbio mara dufu. Jina la namba niliyoitazama linasomeka kwa herufi kubwa NJASI MWAJASI. Ninausoma tena ujumbe wake, zaidi ya mara tatu ninaurudia kuusoma.
“Dobe, hakika umeniudhi sana. Kwani mie nilikuwa nakufikiria uwe mtu wangu mpango wa kando, nikupe maisha uwe vizuri. Lakini umeamua kutembea na Jesca! Hivi hukumuona Jesca kama ana Uume kama wewe, ukaamua kutembea nae? Uke wangu hukuupenda hadi umekwenda kutembea na SHEMALE, kisha natambulishwa kwako kuwa mie wewe ni shemeji yangu! Haya sina neno namba yako nimeiiba katika simu yake. Kwa taarifa yako amekutangaza kuwa umetembea nae, na amenambia kila kitu kuwa mmefumwa na Meneja wako, na kwamba anataka akuajiri ili muendelee kula tunda!”
Ujumbe huu unaniumiza sana, kwani mie sijawahi hata kutembembea nae kwenyewe. Japo ibilisi ameniingia na hakika ningemfanya kweli, kama siyo meneja kuingia. kwani nilikuwa naogopa kutangazwa. Sasa hata jambo lenyewe sijalifanya tayari nishatangazwa!
Ninaamua kuipigia ile simu ya Njasi ili nimuombe radhi lakini pia nimwambie ukweli ulivyo, lakini simu yangu inanambia haina salio!
Natoka mbio hadi nje nayafata maduka saa moja hii asubuhi, lakini maduka bado hayajafunguliwa.
Ninachukia sana kukaa huku kwa wafanya biashara wavivu, kwani ningekuwa nakaa uswahilini hivi maduka ningeyakuta wazi, kwani kuna baadhi ya wenye maduka huwa wanakesha kabisa. Lakini huku maduka hadi igote saa tatu ndiyo yafunguliwe.
Ninarejea nyumbani huku ninamlaani Jesca kwa kunitangaza ndivyo sivyo!
Ninaingia chumbani kwangu, ukumbini nakutana na mama mwenye nyumba wangu ananishangaa.
“Dobe vipi leo mbona umetoka mara unarudi, unaumwa mwanangu?”
Ninamjibu kwa mkato.
“Naam naumwa homa imenishika sana.”
Ninaingia chumbani huku ninalaani tabia yakutaka kufatilia mtu ujue kama mgonjwa au mzima. Ninajilaza kitandani, sura ya Njasi inanijia mawazoni mwangu, ninakumbuka namna alivyokuwa akilia kwa mahaba, namna nilivyokuwa nampagawisha kwa massage, nakumbuka alivyokuwa akipita nilipokuwa nimesimama mie na meneja.
Moyo wangu unaniuma machozi yananilengalenga. Sijui kwa yakini kwa nini nimekuwa ninalia lakini kidume machozi yananitoka.
Mara inanijia akili kuwa nikope katika simu yangu ili nimpigie simu Njasi nimfate alipo, hata akitaka nimrambe miguu ili anisamehee nipo tayari, lakini siyo kuwa mbali nae. Nipo radhi anipe adhabu ikibidi lakini siyo kumkosa.
Haraka ninaishika simu yangu, naanza kubonyeza namba kadhaa ili kuomba mkopo Tigo, lakini nao wananichosha kabisa! Ujumbe unanambia siwezi kutumia huduma ya mkopo kwa vile nina deni bado sijalilipa!
“Shit”
Naitazama simu yangu, nahisi Njasi kama ananisubiri hivi nimpigie simu ili nimwambie ukweli, lakini mtandao unanihujumu. Ninaamua nikaoge kabisa ili kuvuta muda zaidi maduka yafunguliwe nikanunue vocha.
Navua Track yangu niliyolala nayo tangu jana, navaa taulo, nachukua na mswaki, nabeba maji nakwenda bafuni kuoga. Ninaoga taratibu navuta muda ili maduka yafunguliwe. Ninapiga mswaki kisha natoka bafuni. Ninapofika chumbani kwangu, napatwa na mshituko wa mwaka.
Taulo linanidondoka bila kujitambua
“Hee wewe!”
Najikuta natamka bila kutarajia.
“Vaa Taulo lako acha kukaa uchi wewe.”

5

Ninainama naliokota taulo, nakujifunika kwa mbele tu kwani nikileta utaalazi wa kulifunga kiunoni vyombo vitazidi kuonekana bure!
“Pole sana kwa kukushtua namna hiyo. Ila nimekuja kukutazama baada ya jana tangu ulipoondoka kazini hadi leo asubuhi saa kumi na mbili kasoro nakupigia simu, ulikuwa haupo hewani na wewe binaadamu. Kwa kuwa hapa kwako ninapajua tangu siku ile uliyonileta kupaona wakati nakuajiri. Nikaona nije kukutembelea kukujulia hali. Hivyo nilipofika hapa nimemkuta mama mwenye nyumba wako amenikaribisha amenambia wewe unaumwa umekwenda kuoga, ndiyo mie nikaona nikusubiri ndani.”
Meneja ananambia kiasi moyo wangu unarudi katika hali yake ya kawaida japo bado unaenda mbio mapigo yake.
“Jana nilikuwa nimechanganyikiwa sana, kiasi nikazima simu kabisa nimekuja nyumbani moja kwa moja nimelala, sijala wala sijaoga na njaa siisikii hadi sasa. Mie nipo mzima ila bado nakuomba nisamehe meneja nirudishe kazini, kwani mwezi huu ndiyo wa mwisho katika mkataba wangu humu ndani, pesa ya chumba sina, na hapa ninalipa kodi ya miezi sita.”
Ninamwambia meneja hali yangu ilivyo ngumu, lakini ajabu yeye macho yake yote yapo katikati ya mwili wangu!
“Dobe kama unataka urudi kazini hata leo hii, basi nifanyie kazi yangu.”
Ananambia huku ananitazama usoni.
“Kazi gani hiyo bosi?”
Ninamuuliza huku nikijifunga taulo kiunoni kwangu kwa namna ambayo siruhusu maumbile yangu kuonekana.
“Mie katika umri nilionao, sijawahi hata siku moja kufika mwisho ninapokuwa kwenye majambo, hivyo nataka kutoka kwako unifanyie kazi hiyo, kwani unaonekana wewe ni mweledi sana wa mambo hayo, isingekuwa hivyo yule Njasi asingekukubali kutembea nawe. Kwani nina hakika utakuwa mmeshafanyana. Je upo tayari kutekeleza hilo ili urudi kazini?”
Ninamuangalia meneja wangu, maneno anayosema ninaona aibu kumjibu kwa mdomo, ninainamisha uso wangu chini, kisha ninamtazama tu bila kusema kitu.
Mkuyati nao kama uliyokuwa inasubiri kwa hamu jambo hili, unaanza kuliinua taulo na kumfanya meneja wangu atabasamu.
“Dobe hata kama wewe hutaki kunijibu, ninaemtaka keshanipa majibu kuwa yupo tayari. Hakika huyo ndiyo shida yangu hasa. Kwani nimempenda ghafla tu.”
Maneno hayo ya meneja wangu yananizidisha mkazo wa chini kwenye taulo, nahisi kunapiga push up!
Hii itakuja kuniua haki ya nani vile, mie sijala kitu japo njaa siisikii, kazi kubwa yakumkojolesha mtu ambae hajawahi kukojoa nitaifanyaje kama siyo kutafutiana kifo? Na mchezo wa matusi unapendeza sana mkiwa wote mmeshiba. Daima haunogi na njaa.
Meneja ninamuona ulimi wake anaurambisha katika midomo yake, macho yamemlegea, na baridi ya nyege imemshika kwani anabadili mikao kila baada ya sekunde tano!
“Mie nimekubali meneja wangu kwa dhiki nilonayo, ila naomba uniruhusu kitu kimoja tu. Naomba nikanywe japo chai ya Mkandaa, ili nipate nguvu yakukufanyia kazi yako vizuri kwa ufanisi. Nikupe mizungu yote niliyopewa na Ngariba wangu Marehemu Juma Fundi Faraji.”
Ninamwambia nikimtazama usoni kama ameridhia.
“Utakwenda Dobe, ila basi naomba uje uninyonye kidogo, kisha utakwenda kunywa chai, kwani nipo vibaya sana.”
Ananambia huku anapandisha sketi yake juu. Tatizo la meneja wangu, hana mvuto kwa wanaume, kwani yupo Shep less. Mwili wake nakataa kuuelezea nisije kumkosoa muumba bure, ila yataka uwe umelewa hivi ili uweze kufanya mapenzi nae ukojoe. Kwani unaweza usisimame kwa kukosa mvuto kwake.
Lakini ajabu ya Uume wangu ushapandisha bendera juu hauna habari. Kwa kuona mapaja tu yaliyojaa michirizi, na viguu vidogo kama upondo wa Ngalawa.
Hizi Dhakari za hivi, ni majanga kwa kweli kuwa nazo.

HAYA MAJANGA NDIYO HAYOO. DOBE ANATUACHAJE?!
ATATUJIBU KESHO SAA TATU USIKU.




Ludewa yetu na maendeleo yetu posted by barnabas njenjema, kutoka Ludewa
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: