Mbaroni kwa kumchoma mtoto kwa kisu cha moto


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George KyandOLISI mkoani Rukwa inamshikilia mkazi wa eneo la Majengo Manispaa ya Sumbawanga, Rose Mwananzumi, akituhumiwa kumtendea unyama mtoto wake mwenye umri wa miaka sita, kwa kumpiga na kumchoma kwa kisu cha moto na kumsababishia majeraha makubwa mwilini.
Mtoto huyo anasoma darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Majengo katika Manispaa ya Sumbawanga.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando alisema mama huyo anatuhumiwa kutenda unyama huo Septemba 4, mwaka huu, usiku katika eneo hilo.
Akizungumza na gazeti hili, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Majengo, Losko Manase alisema juzi kuwa wanafunzi wenzake walimgundua mtoto huyo (jina linahifadhiwa) akiwa na majeraha makubwa mwilini ndipo wakatoa taarifa kwa walimu.
“Mtoto huyo alituonesha majeraha ya moto mikononi, miguuni, mgongoni na tumboni …. Tulipomhoji alisema mama yake mzazi alimwadhibu kwa kumchoma kwa kisu chenye moto …. ndipo tukamtaarifu Ofisa Mtendaji ili askari mgambo wamkamate mama huyo,” alieleza Mwalimu Mkuu.
Ofisa Mtendaji Kata ya Majengo, Lucy Mwakyusa alikiri kupokea taarifa ya mkasa huo kutoka kwa Mwalimu Mkuu wa Majengo, na alichukua hatua ya kumkamata na kumfikisha kwenye vyombo vya dola.
Akizungumzia mkasa huo, mtoto huo huku akionesha majeraha katika sehemu mbalimbali za mwili, alisema siku hiyo ya tukio hakushinda nyumbani alikuwa akichunga ng’ombe za jirani yao ambapo alirejea nyumbani jioni alitendewa vitendo hivyo




Ludewa yetu na maendeleo yetu posted by barnabas njenjema, kutoka Ludewa
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: