RASMI CLAUDIO BRAVO AJIUNGA NA MAN CITY NA KUWEKA REKODI


Manchester, England.
Manchester City imetangaza kumsajili mlinda mlango Claudio Bravo kutoka FC Barcelona kwa ada ya £17m.
Bravo,33,amejiunga na Manchester City kwa mkataba wa miaka minne na anatarajiwa kushuka dimbani wikendi hii wakati klabu hiyo ya jiji la Manchester itakapokuwa ikipepetana na Westham United.
Bravo anakuwa mlinda mlango wa kwanza kutoka Chile kusajiliwa na klabu inayoshiriki ligi kuu nchini Uingereza.
Bravo alijiunga na FC Barcelona mwaka 2014 akitokea Real Sociedad na ujio wake ndani ya Manchester City umefungua milango kwa mlinda mlango wa klabu hiyo Joe Hart kutimka.
Bravo anakuwa mchezaji wa nane kujiunga na Manchester City tangu klabu hiyo ilipoanzwa kufundishwa na Pep Guardiola baada ya Ilkay Gundogan, Aaron Mooy, Nolito, Oleksandr Zinchenko, Leroy Sane, Gabriel Jesus na Marlos Moreno.



Ludewa yetu na maendeleo yetu posted by barnabas njenjema, kutoka Ludewa
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: