CRISTIANO RONALDO MCHEZAJI BORA WA ULAYA



ronn
Cristiano Ronaldo amewashinda wwachezaji Antoine Griezman na Gareth Bale na kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa Ulaya kwa upande wa wanaume. Ushindi huu umetokana na mafanikio yake msimu uliokwisha huku akiwa ametwaa vikombe vikubwa vya ulaya kwa maana klabu bingwa ulaya na kombe la mataifa ya Ulaya.
Ronaldo pia alikuwa mfungaji bora wa Ulaya huku akiwa wa pili kwa ufungaji katika ligi kuu ya nchini Hispania. Ikumbukwe pia, Ronaldo alifika fainali hizi huku mpinzani wake akiwa ni Antoine Griezman na kumshinda kote ijapokuwa kwenye fainali ambayo Ureno walitwaa ubingwa aliumia mapema sana.
Ronaldo alifunga mabao 51 kwenye mechi 48 msimu uliopita huku akifunga mabao 3 pekee kwenye mashindano ya mataifa ya Ulaya ambapo mchezaji Antoine Griezman alikuwa mfungaji bora.
Yaome maswali na majibu aliyoyajibu Ronaldo baada ya kutwaa tuzo hiyo huku pia akiwapongeza wachezaji wenzake waliofika kwenye hatua ya mwisho ya kinyang’anyiro hiki, Bale na Griezman.
RONA
Katika hatua nyingine mchezaji Ada Hegerberg ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa ulaya kwa upande wa akina dada





Ludewa yetu na maendeleo yetu posted by barnabas njenjema, kutoka Ludewa
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: